Saturday, January 31, 2009

Magufuli alia na wavuvi haramu....

Waziri wa Mifugo na Manendeleo ya Uvuvi, John Mgufuli akitoa tamko juu ya kuanza kwa operesheni ya miezi sita ya kupambana na uvuvi haramu na uvushaji wa mazao ya samaki mipakani. Operesheni hiyo inaanza Januari 30 mwaka huu. Picha na Jube Tranquilino

Mzindakaya amlipua bomu jingine....


Mbunge wa Kwela (CCM), Dk Christant Mzindaka, akiwasilisha hoja binafsi bungeni mjini Dodoma jana juu ya kuingiliwa kwa mamlaka ya bunge kulikofanywa na serikali kupitia wizara ya maliasili na utalalii.

Mzindakaye ameeleza kusikitishwa na uzembe uliofanywa na Waziri wa Maliasili, Shamsa Mwangunga kwa kuwaongezea muda wamiliki wa vitalu vya uwindaji katika hifadhi za taifa kinyume na maagizo ya bunge.

Akitoa maeleo hayo kupitia hoja yake binafsi Mzindakaya alisema kuwa Waziri alikiuka agizo la bunge la kufuta vibali vya uwindajidhidi katika maazimio ya bunge yaliyomtaka kusitisha umiliki wa vitalu vya uwindaji wa kitalii mwishoni mwa mwaka jana na badala yake akawaongezea muda wawindaji hadi mwaka 2012.

Hoja ya Dk Mzindakaya, ambayo iliungwa mkono na wabunge wengi, ilikuwa inaweka wazi kuwa bunge liliamuru vibali vilivyokuwa vinatumika viishie 2009 ili kuanzia 2010 taratibu mpya zisizo za kuiba mapato ya serikali zitumike.

Mzindakaya alilieleza bunge kuwa kwa Waziri Mwangunga alipuuza maazimio ya bunge na kusikiliza ushawishi wa matajiri hao wa kigeni wanaofanya biashara na raslimali za nchi, kupitia vitalu walivyomilikishwa na hatimaye akawaongezea miaka miwili hadi 2012.
Mwangunga aliamriwa kusimamisha vibali vilivyotolewa na wizara yake kwa wawindaji badala ya kuisha mwaka 2012 vifikie ukomo 2010, ili kuanzia hapotaratibu mpya za uwindaji zianze kutekelezwa.

Thursday, January 29, 2009

The Citizen inatisha.....

Wabunge wa kambi ya upinzani, Dr. Wilbrod Slaa na Zitto Kabwe(aliyekaa) wakipitia gazeti la The Citizen bungeni mjini Dodoma..... nilipowauliza waheshimiwa hao kwa pembeni hawakusita kusema kuwa.... wao wapo chama makini hivyo kwanini wasipende kusoma gazeti makini.....?

Upinzani hatujasambaratika hata kidogo

Kambi ya Upinzani Bungeni imekanusha kuwepo kwa mpasuko ndani ya kambi hiyo. Naibu Kiongozi wa upinzani bungeni Dr. Wilbrod Slaa ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Chadema amesema kuwa kambi hiyo bado ipo imara na inauongozi madhubuti.

Akizungumza mjini Dodoma, Dr. Slaa amesema kuwa tofauti zilizopo ni za kawaida kwani kila chana kina mikakati yake hususan ya kisiasa. "Vyema watu wakatofautisha baina ya chama cha siasa na kambi ya upinzani..... kwani tofauti ni kwamba wakiwa ndani ya bunge huendeshwa kwa sheria zaidi wakati nje ya ukumbi wa bunge siasa hutawala," ameeleza Dr. Slaa.

Alieleza kuwa matatizo baina yao hayawezi kuepukika ila kinachofanyika zaidi ni mazungumzo baina yao ili kuzitatua tofauti hizo.

Dr. Slaa amesema kuwa Chadema kitaendeleza ushirikiano wa kisiasa na vyama vya CUF na UDP bali kamwe Chadema hakitaendeleza uhusiano wa mashirikiano na vyama vya siasa vya upinzani vya NCCR-Mageuzi pamoja na TLP.

Wachunguzi wa mambo ya kisiasa wameeleza mgawanyiko unaoweza kutokea katika ushirikiano wa vyama hivyo vya upinzani hususan dalili za kuvunjika kwakwe zilizoanza kujitokeza wakati wa uchaguzi mdogo wa ubunge wa jimbo la Tarime.

Dalili hizo za kutoshirikiana pia zilijitokeza wakati wa uchaguzi mdogo wa jimbo la Mbeya Vijijini ambapo mbali na vyama hivyo kutoafikiana kuweka mgombea mmoja, CUF ilidiriki kuweka pingamizi dhidi ya mgombea wa Chadema.

Akizungumzia suala hilo Dr. Slaa amesema kwa sasa vyama vya CUF, Chadema na UDP vinaendelea na mchakato wa mazungumzo yatakayowezesha kuafikiana jinsi ya kugawana majimbo kulingana na nguvu ya chama husika.

Hata hivyo Dr. Slaa pamoja na kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni Hamad Rashid Mohammed wameeleza matumaini yao kuwa ikiwa sheria mpya ya vyama vya siasa itapitishwa na bunge, itatoa nafasi kwa vyama hivyo kuteua mgombea mmoja bila kuathiri mfumo wala itikadi zao.

Mchungaji akila kiapo

Mbunge wa Mbeya Vijijini Mchungaji Luckson Mwanjali akila kiapo cha uaminifu bungeni mjini Dodoma.

Pinda afafanua kauli


Waziri Mkuu Mizengo Pinda amelieleza bunge mjini Dodoma kuwa kauli yake aliyoitoa mikoa ya kanda ya ziwa hakumaanisha tafsiri iliyochukuliwa na wengi ya kujichukulia sheria mkononi bali alikuwa na lengo la kufikisha ujumbe kwa wauaji wa albino kuwa serikali imedhamiria kupambana nao.

Upinzani walia na Pinda

Kambi ya upinzani bungeni imemtaka Waziri Mkuu Mizengo Pinda kutoa ufafanuzi rasmi bungeni juu ya kauli yake aliyeitoa hivi karibuni akiwa ziarani mikoa ya kanda ya ziwa.

Waziri Mkuu alikaririwa na akiagiza kuwa watu wanaokamatwa wakiua albino nao wauawe papohao.


Kambi hiyo imesema iwapo kiongozi huyo wa serikali bungeni atashindwa kufanya hivyo, itailazimu kambi hiyo kushinikisha ajiuzulu. Hata hivyo, kambi hiyo haikueleza ni njia gani haswa zitatumika kushinikiza suala hilo.

Tuesday, January 27, 2009

Mramba ndani ya bunge


MBUNGE wa jimbo la Rombo mkoani Kilimanjaro ambae anatuhumiwa kwa kesi ya kutumia vibaya madaraka yake akiwa waziri wa fedha Basili Mramba jana aliingia katika ukumbi wa bunge kwa mbwembwe huku wabunge wakionekana kumpa pole na kumkumbatia kila wakati.

Hata hivyo haikuweza kufahamika mara moja iwapo amri ya mahakama iliyomruhusu kwenda kutembelea jimbo lake pia inampa nafasi ya kuhudhuria bungeni.

Mramba aliingia katika ukumbi wa bunge majira ya saa 2:46 asubuhi akiongozana na Waziri wa fedha Mustafa Mkulo aliingia huku baadhi ya wabunge walipomuona walianza kumfuata na kukumbatiana katika hali iliyoonyesha kuwa walikuwa wakimpa pole kwa masahibu yaliyomkuta.

Alipoingia katika ukumbi huo alisimama kwa muda mrefu mlangoni ikwa ndani akizungumza na Benedict Ole-Nangoro ambae ni mbunge wa Kiteto (CCM) huku baadhi ya wabunge wengi wa ccm wakipita na kusalimiana nae na kukumbatiana kwa kila mtu.

Katika hali hiyo haikuweza kufahamika mara moja Mramba na Ole-Nangoro walikuwa wakizungumza kitu gani kwa muda mrefu mlangoni hapo hadi mazungumzo yao yalipokatizwa na sauti iliyoashiria kuwa Spika wa bunge alikuwa anaingia katika ukumbi huo.

Ole-Nangoro ni mmoja wa wabunge walioingia katika bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuziba nafasi za wazi baada ya kifo cha aliyekuwa mbunge wa jimbo la Kiteto Benedict Losulutya mwishoni mwa mwaka 2007 na hivyo sio mbunge wa siku nyingi katika bunge hilo.

Mbunge huyo wa Rombo inasemekana alipewa kibali na Mahakama kwa kutembelea jimbo lake na hata kuhudhuria vikao vya bunge akiwa bado ni mbunge halali wa jimbo hilo ingawa kesi yake bado iko Mahakamani.

Haikuweza kufahamika mara moja ni kwa nini mbunge huyo aliweza kufuatwa na wabunge wengi kutoka katika chama chake (ccm) na kusalimiana nae ingawa dalili zilionyesha kuwa kulikuwa na hali ya kupeana pole na kumuweka katika hali ya ujasiri zaidi katika kesi inayomkabili.

Wakati wa mchana mbunge huyo alitoka katika ukumbi wa bunge mnamo saa 7:03 akiwa amefuatana na naibu spika wa bunge la Jamhuri ya Muungano Anna Makinda huku hali ya kumfuata na kusalimiana nae Mramba ikiwa ni ileile kama aliyoingia nayo asubuhi.

Mramba anatuhumiwa kutumia vibaya madaraka yake akiwa waziri wa fedha wakati wa utawala wa awamu ya tatu chini ya Rais Benjamini Mkapa na kwamba alifikishwa mahakamani pamoja na aliyekuwa waziri wa nishati na madini kwa wakati huo Daniel Yona ambae pia amewahi kuwa waziri wa fedha.

Saturday, January 24, 2009

Usafiri reli ya kati

Baadhi ya wasafiri wakiwahi kupanda katika sehemu ya injini(kichwa) cha treni katika stesheni ya Dodoma wakielekea mikoa ya Tabora, Kigoma na Mwanza....
Wengine hawakuwa na pakuweka mizigo yao zaidi ya kuipachika katika maungio ya mabehewa.....
Ndani kumejaa kinoma... inabidi wengine waning'inie katika milango.....
Kujaza abiria kupita kiasi ndio mtindo wa kila siku.... lakini kwa wasafiri nao.... wanaona bora kufika salama tu....
Kero hii imekuwa ni kubwa na ya muda mrefu.... ijapokuwa imepigiwa kelele na wadau mbalimbali wakiwemo wabunge........ Mambo haya yataisha lini....?

Chuo Kikuu cha Dodoma....si mchezo....

Sura ya mbele ya jengo la utawala la Chuo Kikuu cha Dodoma ambacho ujenzi wake ukikamilika kitakuwa ni mojawapo ya vyuo vikuu vikubwa katika Ukanda wa Afrika....
Jengo hili zamani lilijulikana kama Ukumbi wa Mikutano wa Chimwaga...
Mojawapo kati ya maeneo ambapo vitivo vinaendelea kujengwa... hadi sasa kuna vitivo sita ambavyo kila kimoja kitajitegemea kwa kila kitu.....
Baadhi ya mabweni.... hili pichani ni la kitivo cha sayansi ya jamii.......

Friday, January 23, 2009

Matatizo ya maji vijijini.......

Maji hayo ya kamto dizain ya kabwawa wilayani Kongwa mkoani Dodoma hutumika kwa kunywa na kufulia.....
Ndo kama hivyo tena mifugo nayo humo humo.....
Sijawa na uhakika iwapo hali hii ni salama kwa afya ya wanadamu......

Mambo ya Gadhafi

Ujenzi ukiendelea katika msikiti eneo la Airport karibu na Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma........ Mambo ya Gadhafi hayo....!!!

Chadema kuwasilisha hoja binafsi bungeni

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeeleza nia yake ya kuwasilisha bungeni hoja binafsi inayolenga kuilazimisha serikali kuhakikisha hakuna mtoto atakayekosa fursa ya kusoma kwa sababu ya umasikini wa wazazi wake.

Hatua hiyo ya Chadema imekuja huku wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) wakipinga mchakato wa kudahili wanafunzi upya baada ya vyuo vikuu kufunguliwa.

Katika taarifa yake iliyoitoa jana jijini Dar es Salaam, Chadema imeeleza kusikitishwa kwake na utaratibu wa kudahili upya wanafunzi wa shahada ya kwanza unaoendelea UDSM kutokana na kile ilichokieleza kuwa utaratibu huo ni batili kwa kuwa unakiuka mchakato mzima wa udahili ambao hufanywa na vitivo vinavyotakiwa kuhakiki fomu za mwombaji na kuangalia vigezo, vikiwemo ufaulu wa mwanafunzi katika matokeo ya kidato cha sita au sifa zinazofanana na hizo.

Imeongeza kuwa mwanafunzi akishapata udahili, husajiliwa na si kwamba kinachofuata ni udahili mwingine kama inavyofanyika sasa na kwamba hatua hiyo ni kinyume cha utaratibu na kinalenga kuwaumiza wanafunzi, hasa watoto wa masikini.

Karibu theluthi mbili ya wanafunzi waliorejeshwa nyumbani baada ya chuo hicho kufungwa kutokana na mgomo wa kupinga sera ya uchangiaji gharama za elimu, hawataweza kuendelea na masomo baada ya kutokamilisha masharti ya kurejea chuoni, ikiwa ni pamoja na kulipa sehemu ya ada yao katika kuchangia gharama za masomo.


Bunge kuanza Dom

Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linaanza Mkutano wake wa 14 mjini Dodoma Jumanne wiki ijayo (Januari 27) mwaka huu ambapo miswada mitatu mipya itasomwa na maazimio matatu yanatarajiwa kupitishwa.


Taarifa ya Kamati ya Uongozi ya Bunge imeitaja miswada hiyo kuwa Muswada wa Sheria ya Pembejeo (Fertilizers Act, 2008); Muswada wa Sheria ya Kanuni za Vinasaba vya Binadamu (The Human DNA Regulation Act, 2008) na Supplementary Appropriation Act, 2009 na hatua zake zote.


Miswada itakayosomwa kwa mara ya pili kuwa ni Muswada wa Sheria ya Afya ya Jamii, Muswada wa Sheria ya Wanyamapori ya Mwaka 2008, Muswaada wa Sheria ya Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania, Sheria ya Viwango wa Mwaka 2008 na muswada wa kufanya marekebisho kwenye sheria mbalimbali wa mwaka 2008.


Maazimio matatu ya Bunge yanayotarajiwa kupitishwa ni pamoja na Azimio la Kuridhia Itifaki ya Kuanzisha Tume ya Sayansi na Teknolojia ya Afrika Mashariki; Azimio la Itifaki ya Jumuia ya afrika Masahariki kuhusu kuanzishwa kwa Chombo cha Kusimamia Usalama na Ulinzi wa Anga-2007 na Azimio la Kuridhia Itifaki kuhusu Maendeleo ya Jinsia ya Nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara (SADC).


BAJAJ MAYAI

Mambo ya bajaj mayai.... wadosi wajaribu kukimbizana na soko.....!!!
Ila kwa wale wenzatu wa saridalama......ambao usafiri huu a babaj husaidia sana katika maeneo fulani fulan na hususan kutokana na unafuu wa gharama zake.... sijui zikija za namna hii nauli yake itapanda au....?

Saturday, January 17, 2009

Ajali mingine bwana...!!!

Sura ya lori ikiwa imekunja ndita baada ya kugonga nguzo ya umeme eneo la bahi road.....
Kitara kimeingia nyuma ya lori hilo...... hakuna mtu aliyejeruhiwa katika ajali hiyo......

Uzembe wakati mwingine soo...

Kontena likiwa limeanguka katika kipleft kwenye barabara ya darisalam rodi.... ingawa halikuleta madhara... inaonyesha kuwa halikuwa limefungwa ipasavyo katika lori lilimokuwa.... hata hivyo baaada ya kuangakua hapo... lilikaa kwa takriban siku tatu... jambo ambalo lingeweza kusababisha ajali nyingine... lakini nadhani wahusika waliona kuwa ni sawa tuu....

Watoto wa mitaani ni tatizo kichizi dom

Kijana aishie katika mazingira magumu akiwa amelala katika bustani ya Nyerere mjini Dodoma. Idadi ya watoto kama hawa inazidi kuongezeka mkoani Dodoma ambapo takwimu zinaonyesha kuwa kuna zaidi ya watoto elfu 14 wanaoishi katika mazingira magumu mkoani humu, ambapo asilimia 62 ya idadi hiyo bado wapo mitaani.


Thursday, January 15, 2009

Gari za minadani.....

Jamaa akiwa maeneo ya kikuyu katika barabara ya Dom-Iringa akielekea kwenye minada vijijini akiendelea kusubiri abiria zaidi wakati ambapo ngoma yenyewe ishakula mgizo wa kutosha..... Kwa mtaji huu .....Hivi kweli tutafika...????

mambo ya tekelinalokujia.....!!!

Mafunzo hayo ya jinsi ya kutumia kompyuta kwa hawa nduguzetu ..... picha hii imeorijineti toka SABMiller

Mambo ya habari.....

Mambo ya mawasiliano ya habari yamesaidia kwa kweli kuwakip intach wakazi wa vijijini na dunia jinsi inavyokwenda..... hii dish ni katika kijiji kimoja kinaitwa Mpwayungu....kilometa mingi tu kutoka dom manispaa....

Wednesday, January 14, 2009

Mwana idodomya mwingine na mtandao wa sposssss

Mwana idodomya mwingine Israel Saria anakuletea blog hii mahsusi kwa ajili ya spossss spossss……. bofya katika URL hio hapo....


www.tanzaniasports.com

Blog nyingine ya wana idodomya korea kusini...


Mdau Samson Msambazi aliyepo mjini Seoul, Korea Kusini kafungua Globu ya kuwaunganisha wana Idodomya.. kanifoadia msg ili nami niweze pata wapasha habari wengine juu ya blog hii inaitwa

www.dodoma.ning.com

unawea kufungua na kuangalia, unaweza pia kufowadi msg kwenye hii network na pia kutangaza bule kwenye network hii na pia unaweza kujiunga na wewe pia, nia ni kupashana habari juu ya Dodoma.

Mganga wa jadi anaswa na orodha ya majina ya albino

MGANGA mmoja wa jadi wilayani Chamwino amekamatwa akiwa na orodha ya watu walio na ulemavu wa ngozi (albino).

Mganga huyo alikamatwa na mwenyekiti wa kijiji cha Chinangali ya Pili wilayani Chamwino, Ernest Lesilwa kwa kushirikiana na wananchi wa kijiji chake.

Mwenyekiti huyo alisema kuwa mganga huyo pia alikutwa na fomu zaidi ya 29 ambazo anadaiwa kuwa alikuwa akizitumia kuwatoza waganga wa jadi Sh3,500 za mchango ambao haukueleweka mara moja ulilenga kufanyia kazi gani.

Kutokana na tukio hilo lililotokea Januari 7 mwaka huu katika kijiji hicho, Mwenyekiti Lesilwa alisema kuwa wanakijiji wake walipata shaka baada ya kuona mganga huyo (jina tunalo) akiwachangisha waganga wa jadi wa kijiji chake bila kutoa taarifa.

Mganga huyo alikamatwa majira ya saa 10:30 siku hiyo ya Januari 7 na alikutwa akiwa na mganga mmoja (jina tunalo) anayedaiwa kwenda kukusanya fedha alizodai ni malipo kwa ajili ya kuwaruhusu waganga kufanya kazi zao.

Hata hivyo, akiwa katika eneo hilo pia mganga huyo alimtaka mwenzake kumwonyesha kiganja chake cha mkono ili kubaini iwapo kina alama za "M", jambo lililomfanya mganga huyo wa kijijini kuhoji iweje amsome mkono wake.

"Tulipomkamata tulimpekua katika ofisi ya kijiji na cha kushangaza tulimkuta na kichwa kibichi cha nyoka, kitabu cha Koran, msahafu mmoja, simu aina ya Nokia na chaja yake na fomu 29 za kuchangisha waganga," alisema mwenyekiti huyo.

Pia mwenyekiti huyo anadai kuwa ameshangazwa na kitendo cha baadhi ya waganga wa jadi wa kijijini kwake kukubali kumchangia mtaalamu mwenzao huyo wa tiba, bila ya kujali kama ana vibali vya kufanya hivyo.

Waganga wengine wa jadi wa kijiji cha Chinangali wanaodai kutapeliwa na mganga huyo ni pamoja na Grace Mhukula na Agness Lukuna ambao wanadai walitoa Sh3,500 kila mmoja, ingawa mwenyekiti alipomtaka kuonyesha vibali alitoa nakala.

Wakati wakiendelea na mahojiano hayo mganga huyo alianza kutafuna dawa zake za kienyeji na awali alieleza kuwa ni makosa kutekeleza majukumu yake bila kuwasiliana na uongozi wa kijiji.

Tukio hilo limetokea katika kipindi hiki ambacho kuna hekaheka kila mahali nchini juu ya unyama mkubwa wanaofanyiwa walemavu wa ngozi nchini, wengi wao wanadaiwa kukatwa baadhi ya viungo vyao ili vitumike kwa imani za kishirikina.

Juhudi za kumpata kamanda wa polisi mkoa wa Dodoma, Omary Mganga hazikufanikiwa, lakini taarifa kutoka ndani ya jeshi la polisi mkoani hapa zilithibitisha kukamatwa kwa mganga huyo.

Habari hii imeandikwa na Michael Uledi na kuchapishwa katika gazeti la mwananchi....


Tuesday, January 13, 2009

Jamani mjihadhari na Madereva wa Taxi Dom

Hii mtuka.... ina tinted ndo ilikuwa ikifanza mambo ..... hiyo picha ya chini ni jinsi walivyokuwa wakiziba na nguo kuficha namba baada ya kufanya uhalifu...... soma kipande hicho hapo chini kinachofuata upate niuz ilivyokuwa....
Kwa siku kamba mbili mfululizo majamaa hao waliokuwa takrina watatu wamewaliza akinadada na kinamama kibao.... idadi ya waliokwenda kuripoti polisi juu ya uhalifu hui ilifikia saba....

Jamaa hao waligundua kuwa wanawake ni 'weak and easy target'... basi hujifanya ama wanawapa lift au wanatoa huduma ya tax....

Wakishapanda kinadada hao... na kueleza wanapoelekea... majamaa hao huunganisha juu kwa ju hadi eneo ambalo halina raia kwa wingi na kuwakaba na kuwapora kinadada hao simu, fedha na vidani.

Kwa mujibu wa wanaotuangalizia usalama wa makao makuu yetu.... mtu mmoja ameshatiwa mbaroni kuhusiana na matukio hayo......

Jamaa huyo alikwenda polisi kutoa ripoti kuwa gari yake imeibwa na ndipo polisi walipopata mashaka nae na kumbana zaidi... hatimaye akakiri kuwa alihusika...... gari hiyo ilipopatikana ilikuwa na kitambaa ambacho kilikuwa kikitumika kufunika namba za usajili za nyuma.... damu kidogo katika kiti cha nyuma zilizotoka puani kwa dada mmoja wakati wa zoezi la kumkaba.... pia ilipatikana grander moja walioporwa kimamama wengine na hao hao jamaa.....

Vitu hivyo vyote pamoja na huyo dereva aliweza kutambuliwa na wahanga wa matukio hao wakati wa gwaride la utambulisho..... Msako unaendelea kuwatavuta wenziwake waliokuwa wakitekeleza pamoja uhalifu huo......

Jamani epukeni lift za magari zizisokuwa za kichwa wala miguu... hususan kwa akina dada.... na kwa ushauri wa bure... unapokodi taxi kuwa makini kungalia waliyomo ndani...... usikubali dereva akakwambia kuwa yupo na konda wake katika taxi ..... tani kakambia taxi inaendeshwa au inawahudumu wawili...... iamin zaidi ya dereva pekee.........

ALIYEJUFANYA MTOTO WA JK KORTINI...

Kijana wa miaka 27, Rashid Twali (mbele) mkazi wa Dsm akisindikizwa kwa kortini kujibu mashitaka ya kujifanya mtoto wa JK ili kujipatia nafasi ya mafunzo katika kambi ya JKT Makutupora mkoani Dodoma
Rashid Twalib akiwa ndani ya mahakama
Hapa akirejeshwa rumande baada ya kesi ambayo imeahirishwa....... ila nduguzangu... jinsi ya kupata hizi ajira milioni moja zilizoahidiwa kaaaz kwelkwel.......!!!


Kwa Ufupi... kijana huyo alisonga hadi kambini Makutupora ambapo alipofika kwa geti alimtonya ofisa incharge kwa geti kuwa yeye ni mwana wa JK na kwamba amekuja ili kujiunga na mafunzo ya awali ya JKT kwa kambi hiyo kwani hata CDF anahabari zake.

Sajent aliyekuwepo kwa zamu hapo kwa geti alipata mashaka kidogo akawasiliana na makamanda wake ambao nao waliwasiliana na hedikotaz kupata uhakika, na huko wakawasiliana na wale jamaa wenye jengo lenye kuta nyeupe pembezoni mwa bahari ya hindi kama unaenda vile kwa kushoto.

Jamaa walipowasiliana na mzee mwenzangu ikawa sivyo hivyo, ikabainika kuwa mshkaji anafunga kamba.... hapo ndo soo likaanza na jamaa kufunguliwa chajez.......

Wee huoni hiyo alama

Askari wa Usalama barabarani akimuonya dereva baada ya kukiuka alama ya usalama barabarani (kushoto) inayomuonyesha kuwa hiyo ni njia moja tu..... Hawa ndio madereva wetu wa bongo.....

Hii ndo bongo bwana.....!!

Mshkaji akila ride mitaa ya Dom huku kapakia abiria wawili kinyume na sheria za usalama kwa road hususan kwa vyombo kama hicho kwa picha........

Saturday, January 10, 2009

POLISI DOM VS MTIBWA SUKARI YA MORO

Mlinda mlango wa Mtibwa Sugar ya Morogoro mkiruka juu kuwania mpira na mshambuliaji wa Polisi Dodoma Salim Gilla wakati wa mchezo wa ligi kuu duru la pili iliyochezwa katika Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma. Timu hizo zimetoka sare 1-1.


Mshambuliaji wa Polisi Dodoma Bantu Admin (kulia) akiwania mpira na beki wa Mtibwa Sugar ya Morogoro Idrisa Rajabu wakati wa mchezo wa ligi kuu duru la pili iliyochezwa katika Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma. Timu hizo zimetoka sare 1-1.



Friday, January 9, 2009

NANI KAKWAMBIA KUWA JK HAKASIRIKAGI....???

Samtaim mtu ukiwa siriaz kidogo inafaa.........
Wadau naombeni kapsheni katika ........!!!!

matokeo UWT....

Mke wa Rais Mama Salma Kikwete (kushoto) akimsalimia Mjane wa Mwl Nyerere, Maria

Mwenyekiti mpya wa Jumuiya ya Wanawake Tanzania ya CCM (UWT) Sophia Simba akifurahia ushindi........


Hivi kweli tumeshinda....!!!!
Mwenyekiti mpya wa Jumuiya ya Wanawake Tanzania ya CCM (UWT) Sophia Simba na Makamu wake Asha Bakari Makame(kushoto)

Kampeni UWT zilianza longi.....

Wengine walitumia vilongavonga
Katika kampeni ..... lazima uwe na timu yako bwana

Kabla ya mkutano..... mikakati bado ilikuwa ikiendelea

Tuesday, January 6, 2009

Habari zilizovunjika......Viongozi wa UWT Manyara wapata ajali......

Katibu Mkuu wa UWT mkoa wa Manyara, Verosa Mjema (chini) na Katibu muktasi wake Riziki Rashid Chikoko (juu) wakiwa katika chumba cha wagonjwa mahutuki katika hospitali ya Mkoa wa Dodoma baada ya kupata ajali ya gari katika eneo la chenene, Haneti wilayani Kondoa wakiwa njiani kuja Dodoma katika mkutano mkuu wa jumuiya hiyo. Kwa mujibu wa madaktari, wote wawili wamepata majereha makubwa kichwani na wanatarajiwa leo januari 07 kupelekwa muhimbili kwa matibabu zaidi. Blog hii ya wana idodomya inawatakia ugua pole viongozi hao wa uwt mkoa wa manyara... mwenyezi mungu awajalie wapate pona mapema na kurejea katika ujenzi wa Taifa….



Katibu Mkuu wa UWT Mkoa wa Manyara Verosa Mjema pamoja na katibu muktasi wake Riziki Rashid Chikoko wamejeruhiwa vibaya baada ya kupata ajali ya gari katika eneo la chenene, Haneti wilayani Kondoa jana Januari 06 wakiwa njiani kuja Dodoma kuhudhuria mkutano mkuu wa jumuiya hiyo unaoanza leo Januari 07.


Kwa mujibu wa madaktari katika hsopitali hiyo, Verosa na Riziki wamepata majeraha makubwa kichwani ikiwa ni pamoja na mipasuko wakati riziki ameumia pia jicho lake la kushoto.


Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa Dkt. Jacob Chembele amesema majeruhi hao wanatarajiwa leo Januari 07 kusafirishwa kupelekwa katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa Matibabu zaidi.


Jumla ya watu watano wamejeruhiwa katika ajali hiyo ya gali iliyokuwa na watu sita wakiwahi mkutano huo.


Miongoni mwa wailojeruhiwa ni pamoja Suzan Maliki aliyeumia jicho la kushoto kwa mujibu wa Kaimu Mganga Mfawidhi wa hospitali hiyo ya mkoa, Phillemon Saigodi.

Wengine ni Mwenyekiti wa UWT mkoa wa Manyara Elizabeth Malle na Christina Simon aliyepata majeraha madogo ambapo walitibiwa na kuruhusiwa.


Hata hivyo kwa mujibu wa Dkt. Saigodi mtu wa sita aliyetajwa kwa jina la Mama Chonjela aliyekuwa pamoja na majeruhi hao katika gari hiyo aina ya pajero hakufikishwa hospitali na haikufahamika mara moja iwapo alipata majeraha au laa.