Friday, August 28, 2009

Uzembe mwingine bwana... wee wacha tu...!!!

Gari ikiwa imetupwa kiasi cha mita 50 toka mahala ilipogongwa na kiberenge eneo la majengo mjini Dodoma hivi karibuni wakati dereva akitaka kuwahi kuvuka kabla ya kiberenge hicho kupita.
Baadhi ya mashuhuda wakiangalia gari hilo ambapo hata hivyo hakuna abiria aliyejeruhiwa saaana.....
Mmoja wa walioshughudia ajali hiyo akijaribu kuelezea ilivyotokea....si unajua jinsi tulivyo hodari katika kusimulia.... kama movie vile.....!!!

Thursday, August 27, 2009

Mavituz ya Traffic police huyu.. balaa...!!

Download uone mavitu ya huyu traffic akiongoza magari.....kama angelikuwa bongo.. sidhani kama angelikuwepo hai.....!!!!

Mjihadhari na watu msiowajua mkiwa safarini...!!!

Kijana Meshark Simon akiwa amelala hajitambui jana baada ya kupewa kitu kinachodhaniwa kuchanganywa na dawa za kulevya alipokuwa safarini kutoka Dar es Salaam kwenda Dodoma katika basi la Kilimajnaro Line na kuibiwa vitu alivyokuwanavyo ikiwa ni pamoja na simu ya kiganjani na fedha.
Utingo wa Basi la Kilimanjaro Line akijaribu kumuuliza ilivyotokea kijana Meshark Simon. Jamani abiria mjihadhari na watu msiowajuwa mkiwa safarini....!!!

Wednesday, August 26, 2009

Je hii ni mikogo au taabu ya usafiri...?

Watoto wakiendesha baiskeli katika Bara bara ya Bahi mjini Dodoma jana wakiwa wamepakizana katika hali ambayo inahatarisha usalama wao barabarani.

Tuesday, August 25, 2009

Cycle For Understanding mission....

Eric Silverman akipiga picha ya video waliposimama kwa muda katika hoteli ya Dodoma Hotel....
Aaron Bodansky (kulia) na Eric Silverman wakizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma wakiposimama kwa muda wakiwa njiani kuelekea jijini Nairobi Kenya wakitokea Cape Town, Afrika Kusini kwa kutumia baiskeli, katika kampeni yao ya kubadilisha fikra na mtazamo wa wamarekani juu ya Bara la Afrika. Jamaa hawa wawili ambao nao pia ni Wamarekani wamemaliza safari yao hiyo salama bin salmin.
Hapa Aaron Bodansky akielezea jinsi hali ya safari yao ilivyokuwa tangu walipoingia katika mpaka wa Tanzania hadi kufika Dodoma.

Vibuyu

Mwaha akitafuta wateja wa vibuyu katika mitaa ya mji wa Dom..... babu huyu ni kwa miaka mingi sasa hufanya biashara hiyo.....

Sakata la majambazi Dodoma

Majeruhi aliyetwangwa na kitu kizito kichwani na majambazi wapatao sita ambao baada ya kuteka magari matatu likiwemo basi la abiria, walitoroka kwa kutumia gari ya majeruhi huyo. Kwa mujibu wa Polisi, majambazi hayo yaliuawa na wananchi wenye hasira.
RPC wa Dodoma akikagua baadhi ya vitu zikiwemo simu 25 za kiganjani, mkwanja cash Sh1.95, binduki mbili, mapanga na visu walivyokuwa wanatumia majambazi hayo.

Hapa kamanda akizungumza na wakazi wa Dodoma nje ya chumba cha maiti katika hospitali ya mkoa ambapo miili ya watu hao sita ilikuwa imehifadhiwa.

Monday, August 24, 2009

Uzazi wa Mpango

Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dkt. Julius Kivelia akiwasilisha mada wakati wa mdahalo wa wazi juu ya masuala ya uzazi wa mpango ulioandaliwa na Engender Health na kufadhiliwa na shirika la USAID mjini Dodoma. Huyu Mtaalam anasema kuwa kasi ya ongezeko la Idadi ya Watu nchini Tanzania ni kubwa mno ijapokuwa ukimwi unaendelea kupunguza watu wengi... na kwamba itaongezeka na kufikia watu millioni 90 katika miaka ya 2035 ikiwa hatua madhubuti za uzazi wa mpango hazitachukuliwa.

Ndo zetu....!!

Mwandesha baiskeli akionesha mikogo yake katika mitaa ya dom......

Nyama choma

Mambo ya Dom ndo haya....Hii ilikuwa wakati wa nane nane.... si wajua wana wa idodomya kwa nyama ndo wenyewe...!!

Ngongoti

Ngongoti akionyesha mikogo yake wakati wa maonesho ya nanenane mjini Dodoma.

Kobe mzee

Baadhi ya wakazi wa Dodoma wakiangalia Kobe mwenye umri wa miaka 151 wakati wa maonesho ya nanenane yaliyomalizika hivi karibuni. Wataalam wanasema kuwa Kobe anauwezo wa kuishi kwa takriban miaka 500.

Hongera

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dr. James Nsekela akimkabidhi mwanafunzi wa darasa la saba wa shule ya msingi Kongwa Debora Hongole Baiskeli ikiwa ni zawadi ya usindi katika mitihani ya majaribio kwa masomo ya Hisabati na Sayansi. Zawadi hizo zimetolewa na Benki ya CRDB.