Friday, August 20, 2010

COMPUTER HARD DRIVE DISK ya 19 KWEUSI....

Hii picha ilipigwa mwaka 1956…. It's a hard disk drive back in 1956... with 5 MB of storage. Mnamo mwezi Septemba 1956, Kampuni ya IBM ilizindua a 305 RAMAC, the first 'SUPER' computer with a hard disk drive (HDD) iliyokuwa na uzito wa zaidi ya tani moja na uwezo wa kuhifhadhi data wa 5MB. At least now you have to appreciate a little more ...for the 8 GB memory stick ndani ya mufuko yako....

Tuesday, August 3, 2010

WAKINA HING HONG BALAA

JAMANI HIVI SASA HIZI BODA BODA ZISHAKUWA TATIZO BONGO VIJANA WETU WANAVUNJIKA MNO... KAMA VILE HAITOSHI.. HAWA JAMAA WAMETULETEA HIZI NYINGINE......(MALIZIA NINI KITAKACHOTOKEA)... KITENDO KAMA JINA LAKE VILE..!!

Friday, June 11, 2010

Hii shule iko wapi wajameni..?

Majina mengine ya shule... jamani ni noma... yaweza ata kuathiri wanafunzi wanaosoma hapo.....naambiwa hii skuli ipo Kisumu huko Kenya.... kwa mnaojua at ni kweli....???

Thursday, June 10, 2010

Vuvuzela kuanga kunguruma Sauz

Hii ndo raha ya soka sauz.... bila vuvuzela... soka halipigiki.... Zitaanza kunguruma kwa mwezi mmoja kuanzia hiyo kesho... wakati wa ufunguzi wa 'Weld Kap'

Hiki si kioja cha mwaka...bali ni AIBUU...

Ati hapa maafisa hawa ndo wanajionyesha kufanya kazi yao mbele ya kamanda mkubwa aliyekuwapo akishughudia mechi hiyo....
Shabiki alipandwa na mdadi na kuamua kuingia uwanjani kumkumbatia Kaka wa brazili, ambaye kwa shabiki huo anadai kuwa anamkubali kinoma....... cha kujiuliza ni kwamba jamaa huyo karuka toka eneo la jukwaa hadi kuingia kwa kiwanja(pitch) wanausalama walikuwa wapi... je angelikuwa na kisu.... ama silaha yeyote huku akiwa na nia ovu.. Tanzania ingewekwa wapi katika ramani ya soka hususan masuala ya usalama viwanjani..... Hii ni aibu....

Hapa wanausalama wanaonekana wakiwa wame-relax wakijiburudisha kwa kuangalia samba la wana brazil dhidi ya JK boys.... hawakuwa na habarin kabisaaa juu ya kuangalia usalama wa wachezaji na mashabiki wengine.... inawezekana kitendo cha shabiki hapo juu kuingia uwanjani kilitokana na hawa maafande kutokuwa sirias.....
Picha zote kwa hisani ya Jackson Odoyo....

Huu ni Unyama....

Mtoto (jina tumelihifadhi) mkazi wa Buteko nje kidogo ya mjini Kigoma, akionyesha majeraha ya moto katika nyayo zake alizochomwa hivi karibuni na mama yake mzazi, kwa madai ya kuchelewa kurudi nyumbani. Picha kwa hisani ya mdau Leonard Mubali

Hata hivyo.. kitu kimoja cha kushangaza ni kwamba matukio mengi ya ukatili wa namna kama hii dhidi ya watoto yaliyoripotiwa katika vyombo vya habari yanawahusisha au yamefanywa na akinamama. Wanawake hawa japokuwa wapo mstari wa mbele kudai na kutetea haki za watoto... kwa upande mwingine wamekuwa wakididimiza haki hizo kwa kuwatendea ukatili kama huu... hebu angalia hizi takwimu hapo chini.....

Incidents on Child abuse that shocked nation this year.
Below are some of the incidents of Child brutality by parents or guardians reported in the media recently. However, many other cases go unreported. But one may notice in such events that women, who are mothers, had been mostly reported to have carried out such cruelty to their children.
· May 17 - Police in Ruvuma arrested Asha Salum after she was allegedly slashed and seriously injured her four children using a machete. The reason was that they eat cooked rice she had anticipated to eat herself after imbibing alcohol. One child later died in hospital.
· April 30 – A woman said to be mentally retarded killed her three children with an axe in Longuo Ward in Moshi municipality.
· April 13 - Zuwena Mahamudu, 29, used a red-hot knife to burn her eight-year old Standard two son’s feet for alleged mischief.
· April 19 – A child left as a guarantee for a borrowed dress by her mother in Arusha was seriously burnt in her private parts to compensate for the delay by her mother to return the said piece of cloth.
· April 16 – A 68-year old Amina Mughubi was jailed for three years for burning her three-year old daughter in her private parts using a boiled egg over superstition.
· March 4 - Jesca Maiko, 20, a resident of Geita District in Mwanza Region was arraigned after she strangled to death a three-year old co-wife’s daughter.
· March 11 – A 37-year old Bar maid at Buguruni in Dar es Salaam severely cut her daughter’s legs, hands and buttocks after she forgot to close a door when she went to sleep.
· February 8 - A step mother at Lwega village in Rukwa region severely beat a 7-years old step daughter after she had cooked vegetable seeds. She then hung her up-side-down on a tree where she later died.
· January 13 - A five-year old girl died in Mwanza municipality of injuries sustained after was severe beaten by her mother for soiling her clothes.
· January 8 - Mwanisha Yahaya of Dar es Salaam’s Kimara suburb was charged for applying super glued on the private parts of her seven-year old daughter. The woman was furious on her daughter’s frequent soiling.

Source: The Citizen newpaper.



Wednesday, May 26, 2010

Sheria Mkononi......

(PICHANI CHINI) Askari wa kikosi maalum cha polisi cha (Anti-Robbery) kwa kiswanglish…(Shangazi Jambazi) mkoani Morogoro akimsikitikia kijana (aliyelala chini) baada ya wananchi wenye hasira kumpa kichapo kikali kwa tuhuma za kuiba baiskeli katika mtaa wa Azimio kata ya Kiwanja cha Ndege Manispaa ya Morogoro…....(PICHANI JUU) ..Hata hivyo kijana hiyo hatoweza kushughudia fainali za kombe la dunia mwezi ujao… kwani ndo keshaaga dunia…Hapo akipakizwa katika Londo la Polisi kuelekea mochwale….
Picha hizo kwa hisani ya mdau Juma Mtanda… unaweza kumcheki katika http:/jumamtanda.blogspot.com

Vikundi vya uhamasishaji vyaanza ibuka ..uchaguzi huo waja...

Duuu.. kumbe hawa jamaa wanafani nyingi.......Katibu wa fedha na Uchumi wa CCM Taifa, Amos Makala akitwanga drums ambazo ni moja kati ya vyombo vya muziki vyenye thamni ya Sh10.2 milioni alivyowakabidhi kwa kikundi cha burudani na uhamasishaji cha ‘Sultani Dot Com’ kilichopo kata ya Sultani, manispaa ya Morogoro, Picha kwa hisani ya Samuel Msuya.

Mo Ibrahim kumtangaza rais bora Afrika 2010


Taasisi ya Mo Ibrahimu inatarajia kumtangaza kiongozi bora mstaafu barani Afrika kwa mwaka 2010 ambaye alichaguliwa kidemokrasia na akaiongoza nchi yake kwa kwa mafanikio katika misingi ya utawala bora.

Kiongozi huyo atajulikana Juni 14 na atakuwa wa tatu kufanikiwa kupata tuzo hiyo inayoandamana na donge nono la papo hapo la dola 5 milioni za Kimarekani (sawa na takriban Sh7.3 bilioni za Kitanzania).

Tanzania ina marais wastaafu wawili, Benjamini Mkapa aliyeongoza serikali ya awamu ya tatu (1995-2005) na Ali Hassan Mwinyi, awamu ya pili (1985-1995).

Kwa mujibu wa taarifa Ilioyotolewa na taasisi hiyo Jumatatu wiki hii, rais huyo bora mstaafu wa Afrika atatangazwa mjini London, Uingereza na kamati ya Mo Ibrahim inayoundwa na watu saba waliowahi kuongoza taasisi za kimataifa.

Miongoni mwa wanakamati hao yumo Salim Ahmed Salim aliyewahi kuwa waziri mkuu na katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa ya Afrika (OAU).

Licha ya kiongozi huyo kutunukiwa fedha hizo taslimu, taarifa hiyo inaeleza kwamba maisha yake yote atakuwa akipewa dola 200,000 za Kimarekani (sawa na takriban Shmilioni 260,000 za Kitanzania).

Kiongozi huyo atakuwa ni wa tatu kutunukiwa tuzo hiyo Barani Afrika tangu taasisi hiyo ilipoundwa mwaka 2007.

Waliotunukiwa tuzo hiyo ni rais wa zamani wa Msumbiji, Joaquim Chissano aliyetunukiwa mwaka 2008 na Festus Mogae wa Bostwana (2007).

Mwaka jana kamati hiyo, iliyo chini ya katibu mkuu wa zamani wa Umoja wa Mataifa, Kofi Annan, haikumpata mshindi wa tuzo hiyo.

Taasisi hiyo inaongozwa na mfanyabiashara tajiri wa Sudan, Mo Ibrahim, ambaye amebuni tuzo hiyo kwa lengo la kuimarisha demokrasia na utawala bora Barani Afrika.

Story na Leon Bahati
Source:http://mwananchi.co.tz
Jumatano, 26 May 2010 08:48

Makamba awangurumia makatibu uwenezi CCM

Katibu Mkuu wa CCM Yusuph Makamba, akionyesha vitabu mbalimbali vya maarifa na katiba ya chama mjini Dodoma, Jumanne wiki hii wakati wa ufunguzi wa semina kwa makatibu uwenezi wa CCM kutoka mikoa yote NCHINI. Kulia ni Katibu wa Itikadi na uenezi CCM Kepteni Mstaafu John Chilighati. Picha kwa hisani ya Israel Mgusi... Soma story hapo chini.....

Makamba atamba, aonya makatibu
Jumatano, 26 Mei 2010 08:47

Habel Chidawali, Dodoma

KATIBU mkuu wa CCM, Yusufu Makamba amewaonya makatibu wa siasa na waenezi wa chama hicho, akiwataka kutonunuliwa na wagombea ubunge na akajinasibu kuwa yeye ni mtu anayekwenda na wakati hivyo hawezi kung’olewa katika nafasi hiyo.

Makamba alitoa onyo hilo jana kwenye ukumbi wa NEC Mjini hapa wakati akifungua semina ya siku tatu kwa makatibu hao ambayo itamalizika kesho.

Makamba, ambaye anajulikana kwa ucheshi, pia aliwasimamisha kwenye mkutano huo baadhi ya viongozi wa jumuiya ya wazazi wa mikoa ya Tanga, Morogoro na Dar es salaam, akiwatuhumu kuwa ni vibaraka wa wagombea ubunge.

Katika hotuba yake, Makamba alitamba kuwa njia itakayomuokoa yeye asing’oke katika nafasi yake ni uamuzi wake wa kusoma kwa bidii.

“Mimi nimesoma na ninasoma kila wakati ndiyo maana sibabaiki kabisa... hata ukiniuliza jambo lolote naweza kukuambia kutokana na ukweli kuwa ninakwenda na wakati na nitaendelea kuwa hivyo kila mara ndio maana watu wanasema kuwa ning’atuke, lakini wanaishia kutokuwa na majibu kwa kuwa ninaenda na wakati," alitamba Makamba ambaye watu walitaka aondolewe baada ya CCM kuanguka kwenye uchaguzi mdogo wa jimbo la Tarime.

Aliwataka Makatibu hao kutumia muda wote wa kazi zao katika kupitia vitabu mbalimbali vikiwemo vitabu na vijarida vilivyoandikwa mambo ya CCM ili kujiimarisha katika misingi mizuri ya kupambana na maswali yanayotoka upande wa wapinzani.

Makamba, ambaye amekuwa akimnadi Rais Jakaya Kikwete kuwa ndiye mgombea wa nafasi ya urais kupitia chama hicho, aliwataka viongozi hao kutokuwa vibaraka wa wagombea ubunge.

Kuhusu uchaguzi mkuu ujao, mtendaji huyo mkuu wa chama tawala alisema kuwa kauli mbiu ya mwaka huu ni "ushindi ni lazima ndani ya CCM" na kwamba hilo lazima itekelezwe chini ya usimamizi wa makatibu hao.

“Kwa hiyo mkiondoka hapa msiende kulala; hakikisheni chama kinashinda kweli maana hata tafiti mbalimbali zilizofanywa zimeonyesha kuwa CCM inakubalika kwa asimilia kubwa,” alisema Makamba.

Alisema kuwa mbali na utafiti ambao umeonyesha kuwa Kikwete anakubarika kwa asilimia 85.5, uchaguzi wa serikali za mitaa uliofanyika mwaka jana ulikuwa ni kipimo tosha cha kuonyesha kuwa CCM inakubalika baada ya kushinda kwa asilimia 91.7.

Source:http://mwananchi.co.tz

S

Hii ngoma itakuwa kama ya Liyumba au..????

Watuhumiwa wa kesi ya matumizi mabaya ya madaraka katika Serikali ya awamu ya tatu,kutoka kushoto Basil Mramba, Daniel Yona na Grey Mgonja, wakijadili jambo wakati wakiwa katika chumba cha Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam Jumanne wiki hii, wakisubiri kusikilizwa kwa kesi yao.Picha kwa hisani ya Michael Matemanga

JK ahutubia bunge Afrika Mashariki

Mwenyekiti wa jumuiya Ya Afrika Mashariki, Rais Jakaya Mrisho Kikwete akilihutubia bunge la jumuiya hiyo jijini Nairobi Jumanne wiki hii.Kushoto ni Spika wa bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki Mheshimiwa Abdirahin Abdi.
Rais Jakaya Kikwete (Katikati) akiwa na Spika wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki Abdirahin Abdi (kushoto) pamoja na Spika wa Bunge la Kenya Kenneth Marende(kulia) wakiwa katika viwanja vya Bunge la Kenya Muda mfupi baada ya Rais Kikwete kuwasili na kupigiwa wimbo wa taifa.

Rais Mwai Kibaki wa Kenya akimkaribisha Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Rais Jakaya Kikwete, Ikulu jijini Nairobi jJumanne wiki hii kwa mazungumzo mafupi muda mfupi kabla ya Rais Kikwete kulihutubia bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki. Picha zote kwa hisani ya Ikulu

Tuesday, May 25, 2010

Tanesco yapata bosi mpya

Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) imemteuwa Mhandisi William Geofrey Mhando kuwa Mkurugenzi mpya wa TANESCO. Uteuzi huo unaanza rasmi Juni 1, 2010.

Taarifa iliyotolewa jana (Jumanne) na Idara ya Mawasiliano ya Tanesco imeeleza kuwa Kabla ya uteuzi huo, Mhando alikuwa ni Meneja Mkuu Usambazaji umeme na Masoko katika shirika hilo.

Mhando anachukua nafasi ya aliyekuwa Mkurugenzi wa shirika hilo, Dr. Idris Rashid ambaye muda wake wa uongozi katika shirika hilo umemalizika.

Mhando aliajiriwa na TANESCO October 1987 kama Mhandisi wa umeme, ambapo baadaye alipandishwa na kuwa Mhandisi katika line za umeme.

Mwaka 1990 hadi 1992 aliteuliwa kuwa Meneja wa TANESCO mkoa wa Singida ambapo baadaye mwaka 1992 hadi 1994 alikuwa Meneja wa mkoa wa TANESCO mkoa wa Mbeya.

Vilevile alipandishwa cheo mwaka 1995 na kuwa Mkurugenzi wa Kanda ya Kusini Magharibi hadi mwaka 1999.

Aidha, Mhandisi Mhando ana elimu ya Shahada ya Uzamili (Masters) katika masuala ya umeme aliyoipata Havana Cuba mwaka 1987, vile vile ana elimu aliyoipata katika vyuo mbalimbali ndani na nje ya nchi.

Gari ya JK yabuma wakati wa msafara

Cruiser zilizokuwa zimembeba JK wakati wa ziara yake jumatatu jijini Dar zilibuma maeneo ya BP, Kilwa road(pichani juu) na maeneo ya Kimara, Morogoro road(pichani chini)... (picha kwa hisani ya mdau Michael Jamson)....soma habari zaidi hapo chini......
Gari la JK lazima ghafla barabarani
Tuesday, 25 May 2010 09:33
ZIARA ya Rais Jakaya Kikwete aliyoifanya jana mkoani Dar es Salaam ilipata mushkeli baada ya gari alilotumia kwenye msafara wake kuzimika ghafla mara mbili barabarani.

Gari hilo lilizimika kwa mara ya kwanza katika makutano ya barabara ya Morogoro na Mavurunza wilayani Kinondoni eneo la Kimara Mwisho majira ya saa 7:30 mchana ambako msafara wake ulisimama kwa dakika tatu.

Gari hilo lilizimika tena kama hatua 150 tu kutoka katika makutano hayo na ndipo rais akahamishiwa kwenye gari lingine lililokuwa kwenye msafara huo huku akiwa ananyeshewa mvua.

Tena majira ya saa 10:00 jioni msafara wake uliokuwa ukitokea Keko Toroli wilayani Temeke, ulikwama tena maeneo ya BP barabara ya Kilwa ambako gari hilo jipya nalo lilizimika ghafla.

Tukio hilo la kihistoria nchini, liliwapa wakati mgumu maafisa usalama ambao kila mara gari lilipokuwa limezimika, walishuka kwenye magari yao na kuondoa bendera na ngao.

Kusimama gafla kwa msafara wake eneo la Kimara, kulimlazimisha Waziri wa Maji na Umwagiliaji Profesa Mark Mwandosya kukimbilia eneo alilokuwapo rais huku umati wa watu uliokuwa umejibanza pembeni mwa barabara nao ukisogea karibu.

Ilimchukua takriban dakika mbili kwa maafisa wa usalama wa taifa kupata suluhu ya namna msafara huo utakavyoendelea kutokana na mkanganyiko wa gari ipi kati ya mbili zilizokuwa zinafanana aiangie rais.

Msafara huo uliendelea baada ya Rais Kikwete ambaye alikuwa amevaa shati la kitenge la mikono mirefu na akiwa analowa hasa miguuni kuhamishiwa katika gari jingine huku lile lililoharibika likiwa linasukumwa na umati wa watu hadi pembezoni mwa barabara.

Hata hivyo, baada ya dakika nane gari hilo aina ya Toyota Landcruiser VX V8 lililokuwa na rangi nyeusi, liliwaka baada ya dereva kujaribu kuliwasha kwa zaidi ya mara nne.

Kuzimika kwa gari lake eneo la PB kulifanya msafara wa rais usimame kwa takriban dakika kumi kabla ya kuendelea hadi Ikulu ambako alipumzika kwa muda na kuenda ukumbi wa Karimjee kufanya majumuisho ya ziara yake.
Source: http://mwananchi.co.tz

Monday, May 24, 2010

Hukumu ya Liyumba

Aliyekuwa Mkurugenzi wa Utawala na utumishi wa Benki Kuu ya Tanzania-BOT Amatus Liyumba akipanda basi la magereza tayari kuelekea lupango kutumikia hukumu ya miaka miwili jela baada ya mahakama ya hakimu mkazi kisutu kumpata na hatia ya kutumia vibaya madaraka yake.
Hapa wandugu, jamaa na marafiki wakisikitika baada ya hukumu .........

Liyumba akishauriana na jopo la mawakili wa upande wa utetezi mara baada ya hukumu kutolewa......
Liyumba aki-'riakt' baada ya hukumu kutolewa.....

Hapa ni wakati alipowasili kisutu....... maphotoo kwa hisani ya wadau Fidelis Felix na Venance Nestory......

Vifaru warejea bongo

Baadhi ya maafisa ya shirika la hifadhi za Taifa(TANAPA) na wawakilishi wa mashirika mbali mbali yasiyo ya kiserikali ambayo yanajihusisha na masuala ya uhifadhi, wakiwa wanapokea wanyama aina ya faru toka nchini Afrika ya kusini, jumla ya faru 6 kati ya 32 waliwasili mwishoni mwa wiki katika uwanja wa ndege wa Serengeti. Picha hii kwa hisani ya mdau Mussa Juma

Shule Girini eka yawaka moto

Baadhi ya wandugu wakiangalia majengo ya shule ya 'girini eka' yaliyochomeka.....
Hivi... hii hali inatokana na mgogoro ule wa wanafunzi na uongozi wa shule au ni viboko walivyochapwa madeni....? maswali mengi kuliko majibu...!!

Sunday, March 28, 2010

Usiendeshe karibu na lori lilobeba kontena.... Isijekuwa Kama Kibamba

Lori lilobeba kontena likiwa limepiga chini katika makutano ya barabara......huko mamtoni(ila sio kwa aziz ali wala mtongani).....
Madereva mnatahadharishwa kutoendesha karibu na malori ya namna hii... hususan hapa kwetu bondo salidalama..... mengi ya makontena hayo huwa hayajafungwa ipasavyo..... hiii inanikumbusha ileee ajali ya kimara miaka iileeee.... kipanya (sio masoud) kilivyominjwa na kontena...... hebu endelea kuangalia hizo pix za chini......zimeorijineti toka fun&info@letalites.nets.............

Ajali nyingine majuu kama ya kibamba

Moja kati ya magari mawili yaliyoangukiwa na kontena lililokuwa limebebwa na lori......
Waokoaji wakitafuta mbinu ya kuwachomoa walionasa na wakati huo huo kuwapa huduma ya kwanza........
Hapa ni ka-kiganja tu kanaonekana......
Waokoaji wakimpa huduma ya kwanza moja ya wahanga wa ajali hiyo......
Picha hizi nimetumiwa ktk mail na mdau john mwaipopo... ila zinanesha onesha kama zimeorijineti toka fun&info@letalites.nets.............

Ajali ya Kibamba

Ingawa ajali haina kinga.... lakini hii ni nomaa mazee.....
Sijui tumlaumu Dereva....... au barabara...... au gari lenyewe......????

Wednesday, March 24, 2010

Chopper ya Chadema katika anga za Dom

Helikopta inayotumiwa na chadema katika operesheni sangara ikiwa katika anga za Dodoma... imekuwa ni kivutio kikubwa kwa wakazi wengi wa vitongoji.....

Chadema na Operesheni Sangara Dodoma

Helikopta ikiwasili maeneo ya Kibaigwa wilayani Kongwa...
Wakazi wa Kibaigwa wakiizunguka ....... wengine wanaishangaa... hawajawahi kuiona kwa karibu....

Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe akipokelewa kwa shangwe....


Mpiganaji Mbowe akimwaga sumu jukwaani......

Sumu zikiwaingia vyema wananchi hawa.......

Maadhimisho Siku ya Hali ya Hewa Duniani

Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma Beda Lagule akirusha pulizo ikiwa ni ishara ya maadhimisho ya Siku ya Hali ya Hewa Duniani yaliyofanyika kimkoa katika uwanja wa Ndege mjini Dodoma tarehe 23 March 2010.
Meneja wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Mkoani Dodoma Gaetan Mwikeve akimwonyesha Bw. Beda Lagule baadhi ya vifaa vinavyotumika kupima hali ya hewa wakati wa maadhimisho ya Siku ya Hali ya Hewa Duniani yaliyofanyika kimkoa katika uwanja wa Ndege mjini Dodoma




Majukumu kusaidiana babu....

Wakazi wa Dodoma ambao haikufahamika mara moja uhusiano baina yao wakiwa wamebeba watoto wadogo katika hali inayoonyesha kusaidiana majukumu
Majukumu kusaidiana babu....

Tuesday, March 16, 2010

Dear Mama Musica Saundo kunguruma Dom

Wanamuziki wa Bendi mpya ya Muziki wa Dansi .... wenyewe mwaita masebene..... wakishangilia wakati wa utambulisho kabla ya uzinduzi rasmi utakaofanyika siku ya mkesha wa pasaka......
Waimbaji wakinengua sebene........

Hapo chacha...... Wakisakata mtindo wa 'Makaputura'

Mkurungezi Mkuu wa bendi hiyo.... Josephat Mwashinga akionyesha umahiri wa kucheza sebene wakati wa utambulisho bendi hiyo yenye maskani yake mjini Dodoma......
Hapa "mzee wa makaputura" akionyesha ufundi wa kuimba ingawaje yeye si mwimbaji wa bendi hiyo....... akisaidiwa vocal kwa mbali na rais wa bendi hiyo...Petit Makambo.... mwimbaji na mwanamuziki mkongwe wa siku mingi... toko DRC.....