Monday, February 8, 2010

Air Zara Ikitua jana

Ndege ya shirika la Ndege ya Air Zara ikigusa ardhi ya mji wa Dodoma kuashiria kuzindua safari za ndege hiyo mjini Dom.

Taa kushneh....Uzembe wa madereva

Daladala ikipita karibu na taa ya barabarani iliyopo katika barabara ya Dar es Salaam mjini Dodoma iliyogongwa na gari ambalo halijafahamika mwishoni mwa wiki... si unajua tena kipindi hicho madereva wengi wanakuwa ke..kee..rorooo... Ajali nyingi za nanma hii zimeelezwa kuwa zinazokana na uzembe

Air Zara yazindua safari Dom

Ndege ya Air Zara International aina ya Embrear 120 yenye uwezo wa kubeba abiria 30 ikiwasilis katika uwanja wa ndege wa Dodoma wakati wa uzinduzi wa safari zake. Imeelezwa kuwa uwanja huu umekosa huduma za usafiri ..ati wenyewe wanaziita commercial flights... tangu mwaka 2000.
Waziri wa Miundombinu Dr. Shukuru Kawambwa akimpongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Ndege la Air Zara International, Misha Mango (kushoto)baada ya uzinduzi wa safari za ndege za shirika hizo kutoka Dar es Salaam kwenda Dodoma

Waziri wa Miundombinu Dr. Shukuru Kawambwa akishuka toka katika Ndege la Air Zara International Ndege aina ya Embraer 120 katika uwanja wa ndege mjini Dodoma

Rubani wa Shirika la Ndege la Air Zara International, Jaco De Vries akimuelezea Waziri wa Miundombinu Dr. Shukuru Kawambwa (kushoto) kuhusu mbinu za kurusha ndege

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Ndege la Air Zara International, Misha Mango akimuelezea Waziri wa Miundombinu Dr. Shukuru Kawambwa (kushoto) kuhusu safari za ndege za shirika hilo

Wabunge wa Uganda wakizimia Chuo Kikuu Dom

Baadhi ya wajumbe wa kamati ya bunge ya bajeti ya bunge la Uganda wakimsikiliza makamu mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma wakati walipotembelea chuo hicho hivi karibuni. Hapa wakiwa katika ka-tour kuzunguka chuo hicho kwa basi kwenye barabara ya jumla ya urefu wa kilometa 35 kuzunguka chuo hicho.
Makamu Mkuu wa UDOM akiwapa maelelezo wabunge hao ofisini kwake.

Waheshimiwa hawa kutoka Ugnada wamekubali juhudi hizo... walikuwa wakijiuliza mbona kwao wamelala mnoo.....

Siku ya Kupiga Vita Ukeketaji

Baadhi ya wanaharakati wa kupinga ukeketaji wakiwa katika maandamano kuadhimisha siku ya kupinga Ukeketaji Duniani iliyofanyika kitaifa mjini Dodoma.
Imeelezwa kwamba ingawa hakuna takwimu rasnmi za kitaifa za hivi karibuni, ukeketaji nchini umepungua kwa ujumla toka asilimia 18 mwaka 2002 hadi asilimia 15 mwaka 2008. Mkoa wa Manyara ndio unaoongoza kwa kuwa na asilimia 54 ya vitendo vya ukeketaji.

Madenti wa shule za msingi katika manispaa ya Dodoma nao walikuwemo...