Friday, May 8, 2009

Soka la Bongo

Wakati refa ukiboronga wachezaji wanakukoromea...... huku kwetu idodomya mashabiki ndo wanafanza kazi yao... refa unaletewa nyuki kibao uwanjani.... Taswira hiyo hapo juu ni wakati wa pambano la ligi kuu kati ya wenyeji Polisi na wakata miwa wa Mtibwa morogoro... nyuki walivamia uwanjani mara kadhaa na kufanya wachezaji pamoja na refa kulala chini au kuchukumaa kujinusuru wasijepatwa mandundu....

Different Dates

Different Dates

Hey guys, I don't agree with this one….but still funny..!!


WHITE WOMEN:

First date:

You get to kiss her goodnight.

Second date:

You get to grope all over and make out a bit.

Third date:

You get to have sex but only but only when

she wants to and only in the missionary position.

IRISH WOMEN:

First Date:

You both get blind drunk and have sex.

Second Date:

You both get blind drunk and have sex.

20th Anniversary:

You both get blind drunk and have sex.

ITALIAN WOMEN:

First Date:

You take her to a play and an expensive restaurant.

Second Date:

You meet her parents and her Mom makes spaghetti & meatballs.

Third Date:

You have sex, she wants to marry you & insists on a 3-carat ring.

5th Anniversary:

You already have 5 kids together & hate the thought of having sex.

6th Anniversary:

You find yourself a Mistress.

CHINESE WOMEN:

First date:

You get to buy her an expensive dinner but nothing happens.

Second date:

You buy her an even more expensive dinner. Nothing happens again.

Third date:

You don't even get to the third date and you've already realized nothing

is ever going to happen.

INDIAN WOMEN:

First date:

Meet her parents.

Second date:

Set the date of the wedding.

Third date:

Wedding night.

BLACK WOMEN:

First Date:

You get to buy her a real expensive dinner.

Second Date:

You get to buy her and her girlfriends a real expensive dinner.

Third Date:

You get to pay her rent.

Tenth Date:

She's pregnant by someone other than you.

MEXICAN WOMEN:

First Date:

You buy her an expensive dinner, get drunk on Tequila, and have sex in

the back of her car.

Second Date:

She's pregnant.

Third Date:

She moves in. One week later, her mother, father, her

two sisters, her brother, all of their kids, her grandma, her sister's boyfriend and his

three kids move in and you live on rice and beans for the rest of your life in your home that used to be nice, but now looks like a home along the Tijuana strip.

JEWISH WOMEN:

First Date:

You will have to spend all your money to impress

Second Date:

You will take a loan to keep the image

Third Date:

Your are broke, she finds someone wealthier

ARAB WOMEN:

First Date:

Mother, Father, Brothers, Sisters, Cousins, Aunts, Uncles, Friends and entire Arab community finds out.

Second Date:

Guy is shot dead.

No third date!!!


Hii imetoka kwa mdau Emma Ndossi aliyeko UK.. Shukran...

Thursday, May 7, 2009

Njaa noma..!!!

wahudumu wa msosi katika sherehe moja hivi karibuni baada ya kubanwa na nenge waliamua kuanza kupata msosi kabla ya waalikwa wenginewe katika staili ambayo wasingeshtukiwa kirahisi....

Tuesday, May 5, 2009

Mafua ya ' Ze Hot-chair'

Ati huko kwa pharao wanataka angamiza hawa viumbe wa sir God bureee... wakati huku kwetu sie wala hatuna taaabu nao... tunawachunga malishoni kama hivi uonavyo.... afu baadaye twawapeleka kwa mpareee....!!!

Je waweza hiyo...??!!

Kidole hicho cha pua..... chafya za kufa mtu.....!!!!

Mazingaombwe au mazingara...??

Vijana wakifanza mazingaombwe wakidai ni waganga wa kienyeji (jadi) wenye uwezo wa kutatua shida na matatizo ya watu.... utapeli mtupu... watu kadhaa washalizwa kwa mtindo huo mjini Dom.

Friday, April 3, 2009

Daladala yawaka moto.....

Baadhi ya wakazi wa eneo la Majengo mjini Dodoma wakiangalia gari aina ya Totota Hiace lenye namba za usajili T201ABC lililoteketea kwa moto juzi. Walioshughudia ajali hiyo ambayo hivyo hakuna mtu aliyejeruhiwa wameeleza kuwa chanzo chake ni hitilafu ya umeme........


Hapa viti kushneikgh....tukauze vyuma chakavu......

Kifo hiki kinamashaka...!!!

Baadhi ya wakazi wa mji wa Dodoma wakiwa wamelizunguka gari ya polisi iliyobeba mwili wa mfanyabiashara maarufu mwenye asili ya kiasia, Karim Thawer maarufu kwa jina la Saldina huku bado hawaamini kama kweli katutoka......
Wananchi wakisaidiana na askari kuweka mwili wake kwenye gari(juu)..... (chini) mwili ukitolewa ndani ya duka ambako ndiko kuna ofisi yake......

Hivi ndivyo alivyokutwa marehemu Karim Thawer akiwa ofisini kwake huku amekwisha aga dunia..... Kulikuwa na vitu vyeupe mithili ya povu na mezani pake palikuwa na funguo zake mbalimbali......hotpot ilitokuwa na msosi kiaina... pembeni yake kuna makasha ya dawa... Haikuweza kufahamika mara moja nini kilikuwa chanzo cha kifo chake.... Mwenyezi mungu amlaze mahala pema peponi....

Monday, March 30, 2009

Sita TRL wakamatwa

Wafanyakazi sita wa shirika la reli TRL wanashikiliwa na polisi kuhusiana na ajali ya treni iliyotokea eneo la Msagali katikati ya stesheni ya Gulwe na Igandu wilayani Mpwapwa mkoani Dodoma.

Wnaoshikiliwa ni pamoja na wakuu wa stesheni hizo mbili, dereva wa treni ya mizigo, pamoja na wasaidizi wake watatu.

Serikali imetoa siku tatu kuanzia leo kwa mkuu wa idara ya polisi katika shirika hilo kutoa maelezo ya kina juu ya mazingira yaliyosababisha kutokea kwa ajali hiyo. Manzingira ya awali yanaonyesha kuwepo kwa uzembe pamoja na hujuma uliosababisha kutokea kwa ajali hiyo.

Ajali ya Treni Msagali Mkoani Dodoma

Sehemu ya behewa lililoharibika....
Jamaa wakikata bodi la behewa ili kunasua miili sita iliyokuwamo ndani...
Kipande cha behewa kilichominywa......
Behewa la mizigo lililogongwa....hii treni ya mizigo ilisimama eneo lisilo na stesheni.....ikadaiwa injini iliharibika......dereva wake hakuweka alama yeyote kuonyesha ishara ya ubofu......hakutoa taarifa haraka kwa mkuu wa stesheni alikotoka au anakoenda...Jamani maswali mengi kuliko majibu...!!!!
Injini ya treni ya abiria iliyogonga treni ya mizigo......

Friday, March 27, 2009

JK abadilisha safu ya wakuu wa wilaya

Rais Jakaya Kikwete amefanya mabadiliko katika safu ya Wakuu wa Wilaya nchini ambapo amewateua 15 wapya, kuwastaafisha saba, kuwabadilisha vituo vya kazi wakuu 54 wa wilaya na wawili wakiwekwa benchi wakisubiri kupangiwa kazi nyingine.

Wakuu wapya wa Wilaya walioteuliwa ni Bi. Mercy Silla (Arumeru, Arusha), Bw. Norman Sigalla (Hai, Kilimanjaro), Col. Issa E. Njiku (Misenyi, Kagera), Bi. Angelina Mabula (Karagwe, Kagera), Dkt. Rehema Nchimbi (Newala - Mtwara), Francis Isaac (Mbulu, Manyara), Lt. Col. Benedict K. Kitenga (Rorya, Mara) na Lt. Col. Cosmas Kayombo (Mbarali, Mbeya).

Wengine ni Bw. Christopher Ryoba Kangoye (Kwimba, Mwanza); Bi. Queen Mwanshinga Mlozi (Ukerewe, Mwanza); Bi. Fatuma Mwassa (Mvomero, Morogoro); Bi. Fatma Ally (Nanyumbu, Mtwara); Bw. Juma Solomon Madaha (Tunduru, Ruvuma); Bw. Anatory Choya (Kishapu, Shinyanga) na Bw. Erasto Sima (Korogwe, Tanga).

Waliostaafishwa ukuu wa wilaya (vituo vyao kwenye mabano) ni Bw. Elias Maarugu (Misenyi, Kagera); Bw. Deusdedit Mtambalike (Muleba, Kagera); Bw. David Holela (Babati, Manyara); Bi. Hawa Ngulume (Mbarali, Mbeya); Bw. Mashimba H. Mashimba (Kyela, Mbeya); Col. Peter Madaha (Nyamagana, Mwanza) na Bw. Gilbert Dololo (Kibaha , Pwani).

Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) inaonyesha kuwa Wakuu wa Wilaya wawili, Bw. Patrick Tsere aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Ilala (Dar es Salaam) na Bi. Doreen Kisamo aliyekuwa Uyui (Tabora) wamewekwa bench na watapangiwa kazi nyingine.

Aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Lindi (Lindi) Bw. Martin Shigela kwa sasa ni Katibu Mkuu wa UVCCM wakati aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai (Kilimanjaro) Bi. Husna Mwilima ambaye kwa sasa ni Katibu Mkuu wa UWT.

Sunday, March 22, 2009

Magereza watunukiwa nishani

Kamishna Mkuu wa Jeshi la Magereza, Augustino Nanyaro akimvisha Nishani ya Utumishi Uliotukuka, SSP Kimangano Kivaria wakati wa sherehe fupi ya kutunuku nishani kwa askari na maafisa 301 wa jeshi la Magereza iliyofanyika katika viwanja vya Gereza Kuu la Isanga mjini Dodoma mwishoni mwa wiki.


Hapa Kamishna Mkuu wa Jeshi la Magereza, Augustino Nanyaro akiwapongeza baadhi ya askari magereza baada ya kuwavisha nishani.

Thursday, March 19, 2009

Yako wapi Maisha bora kwa kila Mtz...?

Mwanamama katika kitongoji kimoja mjini Dom akitoka kuteka maji ..... kangani kuna maandishi ya Ari Mpya Nguvu Mpya na Kasi Mpya....... zilotolewa wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu mwaka 2005..... Yako wapi maisha bora kwa kila mtz....? Alihoji mwanamama mwenzie aliyekuwapo nyuma yake baada ya kuniona 'nikimfotobita.....'

Ni kutokuelewa au ukaidi tu...?

Pikipiki ikiwa imeegeshwa eneo ambalo sio egesho katika stesheni la treni mjini Dom.....jamani hii ni ukaidi au kutoelewa.....??

Wednesday, March 18, 2009

malya ahukumiwa miaka 3 jela

Deus Malya akisindikizwa rumande mara baada ya mahakama mjini Dodoma kumtia hatiani kwa makosa mawili ya kuendesha gari kwa uzembe na mwendo kasi na kusababisha ajali iliyosababisha kifo pamoja na kuendesha gari bila leseni. Kwa kosa la kwanza amehukumiwa miaka mitatu wakati kosa la pili ni mwaka mmoja jela. Adhabu hizo mbili zinakwenda pamoja.


Malya alikuwa pamoja na marehemu Chacha Wangwe wakati gari walimokuwa wakisafiria kutoka Dodoma kuelekea Dar es Salaam lilipopata ajali eneo la Pandambili kiasi cha Kilomita 120 kutoka mjini Dodoma.

Tuesday, March 17, 2009

Hii ya MU7 kiboko.....

Hii ya Mu7 nimekutana nao kwa mdau mzee wa simulizi...... ila hii hapa ya mwana Afrika Mashariki mwenzetu kiboko.... manake kwanza yupo kivulini chini ya mti... afu sa mwamvuli wanini tena...?? au kunguru wa zenji nini?

Thursday, March 12, 2009

Mbunge wa Busanda afariki dunia

Mbunge wa Busanda kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi, Kabuzi Faustine Rwilomba amefariki dunia nchini India alikokuwa akitibiwa.

Kwa mujibu wa tovuti ya Bunge, Marehemu Rwilomba alizaliwa tarehe 15 Mwezi Juni 1952 na kupata elimu ya msingi katika shule za msingi Kabugozo 1964-1968 na baadaye Chewamba 1968- 1970.

Marehemu Rwilomba alipata elimu ya sekondari katika shule ya Nsumba 1971-1974 na baadaye kujiunga na chuo cha ualimu cha Korongwe ambapo alipata mafunzo ya daraja la IIIA mwaka 1975 -1976 na kutunukiwa cheti.

Alijunga na Chuo cha Ualimu Butimba mwaka 1981-1983 ambapo alipata Stashahada ya ualimu ya Sanaa (Diploma in Arts) na baadaye Chuo cha Ualimu Morogoro mwaka 1983 -1985 na kupata stashahada ya Elimu (Diploma in Education).

Mwaka 1987-1991 alijiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kupata Shahada ya kwanza ya Ualimu (B.A in Education) kabla ya kuendelea chuoni hapo na kupata Shahada ya juu ya Uzamiri ya Elimu (M.A in Education) mwaka 1993-1995.

Marehemu Rwilomba alianza kazi kama mwalimu daraja la IIIA katika shule ya msingi Hamuyembe mwaka 1975-1981, kabla ya kujiunga na Shule ya Sekondari Nsumba mwaka 1981-1984 akifundisha.

Mwaka 1985-1987 alifundisha katika Chuo cha Ualimu cha Ndala na baadaye kujiunga na Chuo cha Ualimu cha Butimba mwaka 1991-1992 akiwa Mshauri wa Wanafunzi. Mnamo mwaka 1992-1995 alijuinga na Chuo cha Ualimu Tarime kama Makamu Mkuu wa Chuo na baadaye kuwa Mkuu wa Chuo hicho mwaka 1995-2000.

Aliingia katika ulingo wa siasa mwaka 2000 ambapo alichaguliwa kuwa mbunge hadi mwaka 2005 na kisha mwaka 2005 hadi mauti yalipomkuta.

Globu hii inawapa pole wanafamilia, wanabusanda wote, wabunge pamoja na wanandugu jamaa na marafiki.

Mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema peponi… Amen.

Wednesday, March 11, 2009

UVCCM yaalaani beduli lililomchapa kibao mwinyi

Kijana hili sio jambo la kupuuzia..... lazima uelewe nasafi yenu kama vijana.....
Wadhamini hawa wa uvccm wanoteta na mwenyekiti wa umoja huo kabla ya kutoa tamko rasmi kulaani....

UVCCM imetoa tamko leo mjini Dodoma kulaani kitendo cha kijana mmoja kumdhalilisha rais Mstaafu Alhaji kwa kumzaba kibao…. Baraza la umoja huo limeitaka serikali kufanya uchunguzi wa kina juu ya mtu huyo na kiini cha kitendo hicho. Aidha baraza hilo pia limikumbusha vyombo vya usalama kuimarisha ulinzi kwa viongozi wote waliopo madarakani na wastaafu ili kuepusha tendo la aibu kama hilo.

Ikumbukwe wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu mwaka 2005, mheshimiwa JK alikumbana na dhahma kama hii pale mjini Mwanza ambapo jibaba moja lilijipenyeza na kuwapita wanausalama na hatimaye kutinga jukwaani na kutaka kuleta kizaazaa.

Kichapo cha beduli......

Hii ni sawa sawa kwa beduli kama hili....
Hiki kichapo kwa huyo jamaa anayedaiwa kufanya kitendo cha aibu cha kudiriki kumchapa kibao rais mstaafu... nimezinyaka kwa mwanafyale.........nikaona niweke picha bee kuonyesha msisitizo.....

Monday, March 9, 2009

mwanafunzi auawa....

Polisi wakichukua mwili wa Marehemu Willy Nyange(17) ambaye alikutwa ameuawa huku akiwa na majeraha kichani katika eneo la uwanja wa Shule ya sekondari Central mjini Dodoma.

Ubunifu ndo huu..

Nauli zimepanda sasa hivi kila mmoja anabuni usafiri wake ili aokoe gharama pichani wanaonekana wakazi wa chanika wakiwa katika pikipiki yenye matairi matatu, watu wengi waliishangaa kutokana na muundo wake.

Mwananchi -9/17/2008

Saturday, March 7, 2009

Polisi wanasa bangi.....

Polisi wakikagua bangi hiyo......

Basi lenyewe ndo hilo....
Polisi wa kituo cha Kati mjini Dodoma wakikagua bangi baada ya kukamata gunia tano za bangi zilizochanganywa na mkaa, kisha kufungwa vyema na kupuliziwa marashi. Bangi hiyo ilikamatwa Jumanne wiki hii katika basi la Najimunisa lililokuwa likitoka mkoani Mwanza kuelekea Dar es Salaam. Watuhumiwa watatu wanashikiliwa na polisi akiwemo Kondakta wa basi hilo na abiria wawili.

Ndo zetuu.....!!!

Watoto wakiwa wamepakizana katika baiskeli mjini Dodoma jana katika staili ya aina yake bila kujua madhara yanayoweza kuwapata ikiwemo ajali.

Friday, March 6, 2009

Ushikwapo shikamana.....!!!!

Aliimba Jumbe......Penzi ni kikohozi kulificha huliwezi......!!!!

Marehemu Uledi azikwa leo

Waombolezaji wakitoa heshima za mwisho kwa aliyekuwa mwandishi wa habari wa kampuni ya Mwananchi Communications Limited, Marehemu Michael Uledi mjini Dodoma leo. Marehemu Uledi amezikwa leo kijijini kwao Buigiri nje kidogo ya mji wa Dodoma.


Thursday, March 5, 2009

Michael Uledi katutoka....

Mwandishi wa habari wa Magazeti ya Mwananchi katika kituo cha Dodoma Michael Uledi amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika hospitali ya Mirembe alipokuwa amelazwa baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Marehemu Uledi ambaye ameugua TB kwa muda mrefu alizaliwa mnamo mwaka 1969 katika Kijiji cha Buigiri wilaya ya Chamwino.

Marehemu ambaye ameacha Mke na mtoto mmoja atazikwa kesho Ijumaa kijijini kwao Buigiri.

Marehemu Uledi alisoma katika shule ya msingi Buigiri 1977-1983 na baadae mwaka 1986 alijiunga katika shule ya Sekondari ya Chidya wilaya ya Masasi ambako alimaliza kidato cha nne mwaka 1989.


Taarifa za kifo cha Uledi zilitolewa jana na Mke wa marehemu Agness Mzola baada ya kufika hospitalini na kuambiwa kuwa Maiko alikuwa amefariki dunia na ndipo alipoanza kutoa taarifa kwa ndugu na wahusika wa karibu na marehemu.

Mwaka 1990 alijiunga na shule ya sekondari ya Moshi kwa ajili ya masomo ya kidato cha tano na sita ambako alimaliza mwaka 1992 na baadae alijunga katika mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa mkoani Mara ambako alihitimu na kasha alikwenda Jijini Dar Es Salaamu ambako alifanya kazi katika makampuni ya watu binafsi kwa kipindi cha miaka miwili.

Uledi alijiunga na MAMET kwa ajili ya kozi ya Uandishi wa Habari kwa muda wa miezi mitatu na alipomaliza alijiunga na shirika la IPP mwaka 1998 ambapo alipangiwa kituo cha Dodoma akiwa ni Mwandishi wa magazeti ya Nipashe na Gadiani pamoja na Radio One.

Alijiunga na chuo cha Mipango na Maendeleo Vijijini kilichopo mjini Dodoma mwaka 2001 hadi 2003 ambapo alimaliza Shahada ya juu ya Mipango na Maendeleo Vijijini na kufanya kazi kwa muda mfupi katika shirika la Viwanda Vidogo mkoani Dodoma (SIDO) na baadae alihamishiwa katika kituo cha kazi Mtwara.

Mwaka 2004 hadi 2006 alifanya kazi katika Benki ya Exims katika wilaya ya Masasi akiwa ni Meneja Msaidizi wa Bank na baadae alikaa mkoani Morogoro kwa muda mfupi ambako alikuwa akiandika katika gazeti la serikali la Habari Leo.

Januari mwaka 2007 alijiunga na kampuni ya Mwananchi Communications ambao ni wachapishaji wa magazeti ya Mwananchi,Citizen na Mwanasport kazi aliyoifanya hadi mauti yanamchukua.

Alikuwa ni mjumbe katika umoja wa waandishi wa habari za Bunge ambae alikuwa akiwakilisha mkoa wa Dodoma umoja ulioundwa mwaka jana.

Uledi ameacha mke na mtoto mmoja na taratibu za mazishi zinafanyika kwa kushirikiana kati ya kampuni la Mwananchi na ndugu wa marehemu nyumbani kwa Marehemu Nkuhungu mjini Dodoma, mwili wa marehemu unatarajia kusafirishwa leo kwenda Kijijii kwao Buigiri Kilomita 35 kutoka Dodoma mjini ambako mazishi yatafanyika leo saa 5 asubuhi.