Thursday, May 21, 2009

Majambazi Dom wala Sh80

Polisi wakiwasili eneo la tukio muda mchache baada ya watu wanne kupora kiasi cha Sh80 toka kwa mfanyabiashara mwenye asili ya kiasia katika moja ya vituo vyake vya kuuza mafuta mjini Dodoma mwanzoni mwa wiki...
Hapa wakipata maelezo ya awali kutoka kwa watu walioshuhudia tukio hilo jinsi mchezo ulivyochezwa mchana majira ya saa sita hivi...
Hapa wakiangalia maganda ya risasi zilizofyatuliwa na majambazi hao ili kutisha wananchi wasilete longolongo....
Gari lililotumiwa na watu hao wanne wanaosadikiwa kuwa ni majambazi likiwa limetelekezwa eneo la makole mjini Dodoma....
Hapa mdosi aliyeporwa cash akipelekwa wodini kutoka chumba cha upasuaji katika hospitali ya mkoa alipopekekwa kwa matibabu baada ya kutwangwa shaba ya kisigini mguu wa kushoto.... mdodi mwenzie akiwaka kutotaka tukio hilo lisirekodiwe na kuwekwa katika kumbukumbu zatu....