Tuesday, March 16, 2010

Dear Mama Musica Saundo kunguruma Dom

Wanamuziki wa Bendi mpya ya Muziki wa Dansi .... wenyewe mwaita masebene..... wakishangilia wakati wa utambulisho kabla ya uzinduzi rasmi utakaofanyika siku ya mkesha wa pasaka......
Waimbaji wakinengua sebene........

Hapo chacha...... Wakisakata mtindo wa 'Makaputura'

Mkurungezi Mkuu wa bendi hiyo.... Josephat Mwashinga akionyesha umahiri wa kucheza sebene wakati wa utambulisho bendi hiyo yenye maskani yake mjini Dodoma......
Hapa "mzee wa makaputura" akionyesha ufundi wa kuimba ingawaje yeye si mwimbaji wa bendi hiyo....... akisaidiwa vocal kwa mbali na rais wa bendi hiyo...Petit Makambo.... mwimbaji na mwanamuziki mkongwe wa siku mingi... toko DRC.....

Siku ya wanawake....

Wakinamama wakimsaidia msichana ambaye alizidiwa wakati wa sherehe za maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yaliyofanyika kimkoa mjini Dodoma hivi karibuni.... Mwanamana akiwa na watoto wake wa kike wakifuatilia sherehe za maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yaliyofanyika kimkoa mjini Dodoma.......

Mwanamke na Maendeleo

Mwanadada akizunguka katika mitaa ya mji wa Dodoma akitafuta wateja wa karanga huku akiwa na mwanae mgongoni......Ni Kweli "mwanamke na maendeleo tufanye kazi tusonge mbelee......"??

Mbinu mpya ua ukulima wa Zabibu

Mtaalam wa Kilimo cha Zabibu kutoka Afrika Kusini Dirk Bosman akionyesha mbinu mpya za ukulimwa wa zabibu wakati wa ziara ya mafunzo kwa wakulima wa zabibu katika kijiji cha Mpunguzi mjini Dodoma hivi karibuni. Kwa mbinu hizi mpya, mkuliwa anaweza kuvuna tani kati ya nane hadi 13 kwa ekari ikilinganishwa na tani za sasa tatu hadi tano kwa ekari...... Meneja Mkuu wa Kampuni ya Vinjwaji vikali vya Tanzania Distillers Limited (TDL) akiangalia zabibu zinazolimwa mkoani Dodoma. TDL inampango wa kufufua ao la zabibu mkoani Dodoma ambao hutoa takriban hectolitres 120,000 za malighafi inayotengenezewa Wine aina ya Overmeer pamoja na kinywaji kikali aina ya Value.....

Maadhimisho Wiki ya Nssf yaanza

Wanachama wa shirika la mfuko wa hifadhi ya jamii (NSSF) wakipata huduma katika ofisi ya mkoa wa Dodoma ikiwa sehemu ya ni maadhimisho ya wiki ya shirika hilo nchini kote.
Ngoja nikuandikishe ndugu...... uchukue kadi yako.....nawe uwe mwanachama....

Glaukoma yaleta upofu kimya kimya.....

Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini, John Tupa akimvisha miwani Kaundime Seleman wakati wa maadhimisho ya kimkoa ya siku ya Glaukoma Duniani mjini Dodoma hivi karibuni. Mkoani Dodoma pekee takriban watu kati ya 10,000 na 12,000 wamebainika kuugua ugonjwa huo ambapo kati ya hao wagonjwa kati ya 1,500 na 2,000 wamepata upofu kutokana na glaukoma.
Hapa Mkuu huyo wa Wilaya akipimwa uwezo wa jicho kuona taswira na mtaalam wa tiba za macho wakati wa maadhimisho hayo.....