Monday, May 24, 2010

Hukumu ya Liyumba

Aliyekuwa Mkurugenzi wa Utawala na utumishi wa Benki Kuu ya Tanzania-BOT Amatus Liyumba akipanda basi la magereza tayari kuelekea lupango kutumikia hukumu ya miaka miwili jela baada ya mahakama ya hakimu mkazi kisutu kumpata na hatia ya kutumia vibaya madaraka yake.
Hapa wandugu, jamaa na marafiki wakisikitika baada ya hukumu .........

Liyumba akishauriana na jopo la mawakili wa upande wa utetezi mara baada ya hukumu kutolewa......
Liyumba aki-'riakt' baada ya hukumu kutolewa.....

Hapa ni wakati alipowasili kisutu....... maphotoo kwa hisani ya wadau Fidelis Felix na Venance Nestory......

Vifaru warejea bongo

Baadhi ya maafisa ya shirika la hifadhi za Taifa(TANAPA) na wawakilishi wa mashirika mbali mbali yasiyo ya kiserikali ambayo yanajihusisha na masuala ya uhifadhi, wakiwa wanapokea wanyama aina ya faru toka nchini Afrika ya kusini, jumla ya faru 6 kati ya 32 waliwasili mwishoni mwa wiki katika uwanja wa ndege wa Serengeti. Picha hii kwa hisani ya mdau Mussa Juma

Shule Girini eka yawaka moto

Baadhi ya wandugu wakiangalia majengo ya shule ya 'girini eka' yaliyochomeka.....
Hivi... hii hali inatokana na mgogoro ule wa wanafunzi na uongozi wa shule au ni viboko walivyochapwa madeni....? maswali mengi kuliko majibu...!!