Saturday, July 9, 2011

WANAHARAKATI MPO...?!!

Katika hali ambayo kwa kweli sio ya kawaida kuonekana, mzee mmoja akimtumia mlemavu kubeba taka hapo Kimathi Lane jijini Nairobi, Kenya. Katika hili wanaharakati mna kazi..!!

Mshkaji baada ya kupakia mzigo wa taka.... anasepa taratibu.....Nadhani angelikuwa na uwezo wa kuchongesha tolori..asingelimtumia mlemavu huyo na baiskeli yake....

PICHA KUMBUKUMBU BWANA

Mzee(kulia) akiwapanga wanawe watatu (kushoto) ili awapige picha mbele ya jengo la Nation Media Group jijini Nairobi, Kenya, huku wapitanjia wakimshangaa.

FOLENI AFRIKA KAMA KAWA

Msururu wa magari ndani ya jiji la Nairobi, Kenya..... kweli Afrika hali hii kila mahali.

KUFA KUFAANA

Kweli biashara matangazo....ndani ya jiji la Nairobi, Kenya, tangazo la biashara linaloonyesha huduma zitolewazo na kampuni moja inayotoa huduma za maziko..... hapa ukipata huduma unaambiwa karibu tena....!!

sura ya Obama dili kinoma Kenya...!!

Kibao kinachoonyesha huduma ya kupiga picha za passport size kikiwa na picha kama hizo za rais Obama na mkewe Michell, jijini Nairobi, Kenya.

MAPAPARAZI KWA NEWS

Wanahabari wa Nation Media Group kutoka Mwananchi Communications, Tanzania; The Daily Monitor, Uganda na Daily Nation, Kenya wakiangalia vichwa vya habari katika magazeti mbalimbali kwa muuza magazeti jijini Nairobi.

MADEREVA BABA YAO MMOJA

Hapa askari wa kampuni binafsi ya ulinzi akikatiza bila hata ya kumstua dereva kuwa amepaki mahala pasiporuhusiwa hapo Kimathi Lane jijini Nairobi.

Hapa nilifikiri anamuendea kumbe akapitiliza




Dereva akiwa amepaki gari yake kwa Kimathi Lane jijini Nairobi, Kenya, bila hata ya kujali kuwa ameegesha mahala pasiporuhusiwa.... sijua hakuwa anajua kusoma ama aliamua kutoheshimu maelekezo yalokuwepo kwa geti.




Mambo haya ya kuchakachua si mchezo







WANAHABARI MAFUNZONI NAIROBI

Wanahabari wa Nation Media Group kutoka Mwananchi Communications, Tanzania; The Monitor; Uganda na Daily Nation wakiwa katika studio za kituo cha televisheni cha NTV, Nairobi Kenya.


Hapa wakipata maelezo juu ya shughuli za studio kutoka kwa NTV production manager, Phillip Ondeng'.