Eric Silverman akipiga picha ya video waliposimama kwa muda katika hoteli ya Dodoma Hotel....
Aaron Bodansky (kulia) na Eric Silverman wakizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma wakiposimama kwa muda wakiwa njiani kuelekea jijini Nairobi Kenya wakitokea Cape Town, Afrika Kusini kwa kutumia baiskeli, katika kampeni yao ya kubadilisha fikra na mtazamo wa wamarekani juu ya Bara la Afrika. Jamaa hawa wawili ambao nao pia ni Wamarekani wamemaliza safari yao hiyo salama bin salmin.
Hapa Aaron Bodansky akielezea jinsi hali ya safari yao ilivyokuwa tangu walipoingia katika mpaka wa Tanzania hadi kufika Dodoma.
Majeruhi aliyetwangwa na kitu kizito kichwani na majambazi wapatao sita ambao baada ya kuteka magari matatu likiwemo basi la abiria, walitoroka kwa kutumia gari ya majeruhi huyo. Kwa mujibu wa Polisi, majambazi hayo yaliuawa na wananchi wenye hasira.
RPC wa Dodoma akikagua baadhi ya vitu zikiwemo simu 25 za kiganjani, mkwanja cash Sh1.95, binduki mbili, mapanga na visu walivyokuwa wanatumia majambazi hayo.
Hapa kamanda akizungumza na wakazi wa Dodoma nje ya chumba cha maiti katika hospitali ya mkoa ambapo miili ya watu hao sita ilikuwa imehifadhiwa.