Wednesday, July 1, 2009

Polisi wakamata SMG


Ofisa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Mkoani Dodoma (RCO) akionyesha bunduki aina ya SMG yenye nambari NM 181739 iliyokamatwa toka kwa majambazi mjini Dodoma ikiwa na risasi 21. Watu kadhaa wanashikiliwa kuhusiana na matukio hayo ya uhalifu wa kutumia silaha mkoani humo.

Chizi atinga eneo la bunge

Kijana Steven Onesmo (25) aliyetinga kinyume cha taratibu katika eneo la viwanja vya bunge mjini Dodoma na kutishia kushambulia walinzi kwa kisu akidhibitiwa na wanausalama.
Hapa akitiwa katika londo la wana usalama kuelekea kituoni...

Shughuli ya kumpakia haikuwa ndogo.... kijana hiyo ambaye inasadikiwa kuwa ni chizi alileta maroroso mno.,...

Azaki bungeni maonesho

Meneja Habari wa umoja wa mashirika yasiyo ya kiserikali (TANGO) Zaa Twalangeti (kulia) akitoa maalezo wa baadhi ya watu waliotembelea banda ya asasi hiyo wakati wa maonesho ya asasi za kiraia katika viwanja vya bunge mjini Dodoma.

Mbilia alivyoiwapagawisha waheshimiwa

MbiliaBel akionesha mauno alipotumbuiza waheshimiwa katika viwanja vya jengoni mwao mjini idodomya.
Hapa akiweka madoido katika wimbno wake mpya 'mobali ya bebe'

Hapa akicheza na waheshimiwa wakati wa onesho hilo......

Spika naye yumoo.....!! hapa ni baada ya kuombwa na mbilia kupanda kwa stage....

Maisha plus watinga bungeni

Mshindi wa shindano la onesho la luninga la Maisha Plus Abdul (kulia) akiwa na watayarishaji wa shindano hilo wakifurahia jambo na Naibu waziri wa Fedha Omar Yusuf Mzee (kushoto) wakati walipotembelea bungeni mjini Dodoma jana. Katikati ni Mbunge wa Mchinga Mudhihir Mudhihir.