Monday, March 30, 2009

Sita TRL wakamatwa

Wafanyakazi sita wa shirika la reli TRL wanashikiliwa na polisi kuhusiana na ajali ya treni iliyotokea eneo la Msagali katikati ya stesheni ya Gulwe na Igandu wilayani Mpwapwa mkoani Dodoma.

Wnaoshikiliwa ni pamoja na wakuu wa stesheni hizo mbili, dereva wa treni ya mizigo, pamoja na wasaidizi wake watatu.

Serikali imetoa siku tatu kuanzia leo kwa mkuu wa idara ya polisi katika shirika hilo kutoa maelezo ya kina juu ya mazingira yaliyosababisha kutokea kwa ajali hiyo. Manzingira ya awali yanaonyesha kuwepo kwa uzembe pamoja na hujuma uliosababisha kutokea kwa ajali hiyo.

Ajali ya Treni Msagali Mkoani Dodoma

Sehemu ya behewa lililoharibika....
Jamaa wakikata bodi la behewa ili kunasua miili sita iliyokuwamo ndani...
Kipande cha behewa kilichominywa......
Behewa la mizigo lililogongwa....hii treni ya mizigo ilisimama eneo lisilo na stesheni.....ikadaiwa injini iliharibika......dereva wake hakuweka alama yeyote kuonyesha ishara ya ubofu......hakutoa taarifa haraka kwa mkuu wa stesheni alikotoka au anakoenda...Jamani maswali mengi kuliko majibu...!!!!
Injini ya treni ya abiria iliyogonga treni ya mizigo......