Monday, August 24, 2009

Uzazi wa Mpango

Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dkt. Julius Kivelia akiwasilisha mada wakati wa mdahalo wa wazi juu ya masuala ya uzazi wa mpango ulioandaliwa na Engender Health na kufadhiliwa na shirika la USAID mjini Dodoma. Huyu Mtaalam anasema kuwa kasi ya ongezeko la Idadi ya Watu nchini Tanzania ni kubwa mno ijapokuwa ukimwi unaendelea kupunguza watu wengi... na kwamba itaongezeka na kufikia watu millioni 90 katika miaka ya 2035 ikiwa hatua madhubuti za uzazi wa mpango hazitachukuliwa.

Ndo zetu....!!

Mwandesha baiskeli akionesha mikogo yake katika mitaa ya dom......

Nyama choma

Mambo ya Dom ndo haya....Hii ilikuwa wakati wa nane nane.... si wajua wana wa idodomya kwa nyama ndo wenyewe...!!

Ngongoti

Ngongoti akionyesha mikogo yake wakati wa maonesho ya nanenane mjini Dodoma.

Kobe mzee

Baadhi ya wakazi wa Dodoma wakiangalia Kobe mwenye umri wa miaka 151 wakati wa maonesho ya nanenane yaliyomalizika hivi karibuni. Wataalam wanasema kuwa Kobe anauwezo wa kuishi kwa takriban miaka 500.

Hongera

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dr. James Nsekela akimkabidhi mwanafunzi wa darasa la saba wa shule ya msingi Kongwa Debora Hongole Baiskeli ikiwa ni zawadi ya usindi katika mitihani ya majaribio kwa masomo ya Hisabati na Sayansi. Zawadi hizo zimetolewa na Benki ya CRDB.