Thursday, June 10, 2010

Hiki si kioja cha mwaka...bali ni AIBUU...

Ati hapa maafisa hawa ndo wanajionyesha kufanya kazi yao mbele ya kamanda mkubwa aliyekuwapo akishughudia mechi hiyo....
Shabiki alipandwa na mdadi na kuamua kuingia uwanjani kumkumbatia Kaka wa brazili, ambaye kwa shabiki huo anadai kuwa anamkubali kinoma....... cha kujiuliza ni kwamba jamaa huyo karuka toka eneo la jukwaa hadi kuingia kwa kiwanja(pitch) wanausalama walikuwa wapi... je angelikuwa na kisu.... ama silaha yeyote huku akiwa na nia ovu.. Tanzania ingewekwa wapi katika ramani ya soka hususan masuala ya usalama viwanjani..... Hii ni aibu....

Hapa wanausalama wanaonekana wakiwa wame-relax wakijiburudisha kwa kuangalia samba la wana brazil dhidi ya JK boys.... hawakuwa na habarin kabisaaa juu ya kuangalia usalama wa wachezaji na mashabiki wengine.... inawezekana kitendo cha shabiki hapo juu kuingia uwanjani kilitokana na hawa maafande kutokuwa sirias.....
Picha zote kwa hisani ya Jackson Odoyo....

No comments: