Wednesday, March 11, 2009

UVCCM yaalaani beduli lililomchapa kibao mwinyi

Kijana hili sio jambo la kupuuzia..... lazima uelewe nasafi yenu kama vijana.....
Wadhamini hawa wa uvccm wanoteta na mwenyekiti wa umoja huo kabla ya kutoa tamko rasmi kulaani....

UVCCM imetoa tamko leo mjini Dodoma kulaani kitendo cha kijana mmoja kumdhalilisha rais Mstaafu Alhaji kwa kumzaba kibao…. Baraza la umoja huo limeitaka serikali kufanya uchunguzi wa kina juu ya mtu huyo na kiini cha kitendo hicho. Aidha baraza hilo pia limikumbusha vyombo vya usalama kuimarisha ulinzi kwa viongozi wote waliopo madarakani na wastaafu ili kuepusha tendo la aibu kama hilo.

Ikumbukwe wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu mwaka 2005, mheshimiwa JK alikumbana na dhahma kama hii pale mjini Mwanza ambapo jibaba moja lilijipenyeza na kuwapita wanausalama na hatimaye kutinga jukwaani na kutaka kuleta kizaazaa.

No comments: