Tuesday, May 25, 2010

Tanesco yapata bosi mpya

Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) imemteuwa Mhandisi William Geofrey Mhando kuwa Mkurugenzi mpya wa TANESCO. Uteuzi huo unaanza rasmi Juni 1, 2010.

Taarifa iliyotolewa jana (Jumanne) na Idara ya Mawasiliano ya Tanesco imeeleza kuwa Kabla ya uteuzi huo, Mhando alikuwa ni Meneja Mkuu Usambazaji umeme na Masoko katika shirika hilo.

Mhando anachukua nafasi ya aliyekuwa Mkurugenzi wa shirika hilo, Dr. Idris Rashid ambaye muda wake wa uongozi katika shirika hilo umemalizika.

Mhando aliajiriwa na TANESCO October 1987 kama Mhandisi wa umeme, ambapo baadaye alipandishwa na kuwa Mhandisi katika line za umeme.

Mwaka 1990 hadi 1992 aliteuliwa kuwa Meneja wa TANESCO mkoa wa Singida ambapo baadaye mwaka 1992 hadi 1994 alikuwa Meneja wa mkoa wa TANESCO mkoa wa Mbeya.

Vilevile alipandishwa cheo mwaka 1995 na kuwa Mkurugenzi wa Kanda ya Kusini Magharibi hadi mwaka 1999.

Aidha, Mhandisi Mhando ana elimu ya Shahada ya Uzamili (Masters) katika masuala ya umeme aliyoipata Havana Cuba mwaka 1987, vile vile ana elimu aliyoipata katika vyuo mbalimbali ndani na nje ya nchi.

No comments: