Monday, August 22, 2011

Polisi mkoani Kigoma yakamata 52 katika operesheni

 Bangi iliyokamatwa na polisi mkoani Kigoma
Jeshi la Polisi mkoani Kigoma linawashikilia watu 52 kwa tuhuma mbalimbali zikiwemo za ujambazi wa kutumia silaha na wizi wa vocha za simu za mkononi zenye thamani ya karibu shilingi milioni 63.2.
Kamanda wa Polisi mkoani Kigoma ACP Fraisser Kashai, amesema kuwa watuhumiwa 21 wamekamatwa katika wilaya ya Kigoma mjini, watuhumiwa 18 wamekamatwa katika wilaya ya Kasulu na wengine 13 katika wilaya ya Kibondo. Picha/ Pardon Mbwate, PT

No comments: