Friday, March 27, 2009

JK abadilisha safu ya wakuu wa wilaya

Rais Jakaya Kikwete amefanya mabadiliko katika safu ya Wakuu wa Wilaya nchini ambapo amewateua 15 wapya, kuwastaafisha saba, kuwabadilisha vituo vya kazi wakuu 54 wa wilaya na wawili wakiwekwa benchi wakisubiri kupangiwa kazi nyingine.

Wakuu wapya wa Wilaya walioteuliwa ni Bi. Mercy Silla (Arumeru, Arusha), Bw. Norman Sigalla (Hai, Kilimanjaro), Col. Issa E. Njiku (Misenyi, Kagera), Bi. Angelina Mabula (Karagwe, Kagera), Dkt. Rehema Nchimbi (Newala - Mtwara), Francis Isaac (Mbulu, Manyara), Lt. Col. Benedict K. Kitenga (Rorya, Mara) na Lt. Col. Cosmas Kayombo (Mbarali, Mbeya).

Wengine ni Bw. Christopher Ryoba Kangoye (Kwimba, Mwanza); Bi. Queen Mwanshinga Mlozi (Ukerewe, Mwanza); Bi. Fatuma Mwassa (Mvomero, Morogoro); Bi. Fatma Ally (Nanyumbu, Mtwara); Bw. Juma Solomon Madaha (Tunduru, Ruvuma); Bw. Anatory Choya (Kishapu, Shinyanga) na Bw. Erasto Sima (Korogwe, Tanga).

Waliostaafishwa ukuu wa wilaya (vituo vyao kwenye mabano) ni Bw. Elias Maarugu (Misenyi, Kagera); Bw. Deusdedit Mtambalike (Muleba, Kagera); Bw. David Holela (Babati, Manyara); Bi. Hawa Ngulume (Mbarali, Mbeya); Bw. Mashimba H. Mashimba (Kyela, Mbeya); Col. Peter Madaha (Nyamagana, Mwanza) na Bw. Gilbert Dololo (Kibaha , Pwani).

Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) inaonyesha kuwa Wakuu wa Wilaya wawili, Bw. Patrick Tsere aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Ilala (Dar es Salaam) na Bi. Doreen Kisamo aliyekuwa Uyui (Tabora) wamewekwa bench na watapangiwa kazi nyingine.

Aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Lindi (Lindi) Bw. Martin Shigela kwa sasa ni Katibu Mkuu wa UVCCM wakati aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai (Kilimanjaro) Bi. Husna Mwilima ambaye kwa sasa ni Katibu Mkuu wa UWT.

No comments: