Monday, February 8, 2010

Air Zara yazindua safari Dom

Ndege ya Air Zara International aina ya Embrear 120 yenye uwezo wa kubeba abiria 30 ikiwasilis katika uwanja wa ndege wa Dodoma wakati wa uzinduzi wa safari zake. Imeelezwa kuwa uwanja huu umekosa huduma za usafiri ..ati wenyewe wanaziita commercial flights... tangu mwaka 2000.
Waziri wa Miundombinu Dr. Shukuru Kawambwa akimpongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Ndege la Air Zara International, Misha Mango (kushoto)baada ya uzinduzi wa safari za ndege za shirika hizo kutoka Dar es Salaam kwenda Dodoma

Waziri wa Miundombinu Dr. Shukuru Kawambwa akishuka toka katika Ndege la Air Zara International Ndege aina ya Embraer 120 katika uwanja wa ndege mjini Dodoma

Rubani wa Shirika la Ndege la Air Zara International, Jaco De Vries akimuelezea Waziri wa Miundombinu Dr. Shukuru Kawambwa (kushoto) kuhusu mbinu za kurusha ndege

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Ndege la Air Zara International, Misha Mango akimuelezea Waziri wa Miundombinu Dr. Shukuru Kawambwa (kushoto) kuhusu safari za ndege za shirika hilo

No comments: