Monday, February 8, 2010

Siku ya Kupiga Vita Ukeketaji

Baadhi ya wanaharakati wa kupinga ukeketaji wakiwa katika maandamano kuadhimisha siku ya kupinga Ukeketaji Duniani iliyofanyika kitaifa mjini Dodoma.
Imeelezwa kwamba ingawa hakuna takwimu rasnmi za kitaifa za hivi karibuni, ukeketaji nchini umepungua kwa ujumla toka asilimia 18 mwaka 2002 hadi asilimia 15 mwaka 2008. Mkoa wa Manyara ndio unaoongoza kwa kuwa na asilimia 54 ya vitendo vya ukeketaji.

Madenti wa shule za msingi katika manispaa ya Dodoma nao walikuwemo...

No comments: