Thursday, January 29, 2009

Upinzani walia na Pinda

Kambi ya upinzani bungeni imemtaka Waziri Mkuu Mizengo Pinda kutoa ufafanuzi rasmi bungeni juu ya kauli yake aliyeitoa hivi karibuni akiwa ziarani mikoa ya kanda ya ziwa.

Waziri Mkuu alikaririwa na akiagiza kuwa watu wanaokamatwa wakiua albino nao wauawe papohao.


Kambi hiyo imesema iwapo kiongozi huyo wa serikali bungeni atashindwa kufanya hivyo, itailazimu kambi hiyo kushinikisha ajiuzulu. Hata hivyo, kambi hiyo haikueleza ni njia gani haswa zitatumika kushinikiza suala hilo.

No comments: