Ndege ya shirika la Ndege ya Air Zara ikigusa ardhi ya mji wa Dodoma kuashiria kuzindua safari za ndege hiyo mjini Dom.
Daladala ikipita karibu na taa ya barabarani iliyopo katika barabara ya Dar es Salaam mjini Dodoma iliyogongwa na gari ambalo halijafahamika mwishoni mwa wiki... si unajua tena kipindi hicho madereva wengi wanakuwa ke..kee..rorooo... Ajali nyingi za nanma hii zimeelezwa kuwa zinazokana na uzembe
Ndege ya Air Zara International aina ya Embrear 120 yenye uwezo wa kubeba abiria 30 ikiwasilis katika uwanja wa ndege wa Dodoma wakati wa uzinduzi wa safari zake. Imeelezwa kuwa uwanja huu umekosa huduma za usafiri ..ati wenyewe wanaziita commercial flights... tangu mwaka 2000.
Waziri wa Miundombinu Dr. Shukuru Kawambwa akimpongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Ndege la Air Zara International, Misha Mango (kushoto)baada ya uzinduzi wa safari za ndege za shirika hizo kutoka Dar es Salaam kwenda Dodoma
Baadhi ya wanaharakati wa kupinga ukeketaji wakiwa katika maandamano kuadhimisha siku ya kupinga Ukeketaji Duniani iliyofanyika kitaifa mjini Dodoma.
Imeelezwa kwamba ingawa hakuna takwimu rasnmi za kitaifa za hivi karibuni, ukeketaji nchini umepungua kwa ujumla toka asilimia 18 mwaka 2002 hadi asilimia 15 mwaka 2008. Mkoa wa Manyara ndio unaoongoza kwa kuwa na asilimia 54 ya vitendo vya ukeketaji.
Madenti wa shule za msingi katika manispaa ya Dodoma nao walikuwemo...